0


KIKUNDI cha Marafiki wa Waziri Mkuu mstafu,Edward Lowassa Kanda ya Ziwa,wametoa msaada wa magodoro,maji,mafuta na juice kwenye shule ya msingi Mwisenge wanaposoma wanafunzi wenye ulemavu wa ngozi na wasio ona.

Kabla ya kukabidhi misaada hiyo shuleni hapo,marafiki hao walitembea kilometa 3 kutoka Musoma mjini hadi kwenye shule hiyo,kuungana na Lowassa kulaani na kupinga mauaji na ukatili wanaofanyiwa walemavu wa ngozi aliyoyafanya hivi karibuni jijini Dar es salam.

Akikabidhi msaada huo kwa mwalimu mkuu wa shule hiyo Elias Makoro,Katibu wa kikundi hicho,Marwa Silvanus,alisema kutokana na kuguswa na moyo alio nao Lowassa wameamua kumuunga mkono kwa vitendo wakiwa marafiki wake.

Alisema fedha ambazo zimenunulia magodoro pamoja na misaada mingine waliyoitoa,imetokana na michango yao ambayo wamejichangisha wenyewe katika kuunga mkono jitihada zake ambaazo amekuwa akizifanya siku zote katika kupambana na masuala mbalimbali ya kijamii hususani ukatili kwa watu wenye albinism.

Marwa alisema wapo watu ambao pembeni wanadai huenda kinachofanywa ni fedha kutoka kwa mtu kwa lengo la kushawishi jambo ambalo alilipinga na kudai ni moyo wao bila kushawishiwa uliofanya kujichangisha fedha na kutoa misaada hiyo.

Alisema  wao  kama  kikundi  cha  kijamii  wameamua  kutoa  msaada  huo  wa  magodoro  kwa  watoto   wenye  albinism  katika  shule  hiyo  ili  kuunga mkono  matembezi   ya  kupinga  changamoto   zinazowakabili   watu  wenye albinism   ambayo  yaliongozwa  na  waziri  mkuu  mstaafu  edward  lowasa  hivi  karibuni.

“Yanaweza yakatokea maneno kwamba tumepewa fedha kuja kutoa misaada hii hapa shuleni,napenda kuwahakikishi hii ni michango yetu tuliyojuitoa sisi wenyewe na si dhani kama leo mheshimiwa Lowassa anajua kama sisi tumekuja shuleni hapa.

“Sisis tunamkubali Lowassa na tunaunga mkono jitihada zake anazozifanya katika taifa hili na kusudio lake la kutaka kila mtanzania naondokana na unyonge,na kama tungekuwa tumepewa fedha hapa leo tungetoa msaada mkubwa zaidi ya huu ambao tumeutoa leo,”alisema Marwa.

Mmoja wa watu wa kikundi hicho kutoka mkoa wa Mwanza,Kaloli William,alisema wataendelea kuunga mkono jitihaza za Waziri Mkuu Mstafu anazozifanya licha ya kuwepo kwa changamoto ambazo zinazungumzwa.
  
 
Akipokea msaada huo,Mwalimu  mkuu  wa  shule  hiyo ,Elias  Makoro,alisema ni  vyema jamii  na  makundi  mbalimbali  ya  kijamii  yakaendelea  kutoa  misaada  mbalimbali  ili  kuweza  kuwasaidia  wanafunzi  hao  kusoma  katika mazingira  mazuri  na  kuitaka  jamii  kutowatenga  watoto  hao.
 
Alisema msaada huo ni mkubwa kwao lakini  ukosefu  wa  vifaa  vya kujifunzia  pamoja  na  upungufu wa  mabweni  ya wavulana  na wasichana  kwa  wanafunzi  wenye mahitaji  maalum  hasa  kwa wanafunzi  wenye ulbinism  katika  shule  ya msingi Mwisenge B, ni moja   ya  changamoto kubwa   ambazo  zinaikabili  shule  hiyo   ambayo  alisoma  Baba   wa  Taifa Hayati   Mwalimu  Julius Kambarage  Nyerere. 

Kwa upande wake,Afisa Elimu ya Msingi Manispaa ya Musoma,Joakim Machera,alishukuru kikundi hicho kwa msaada walioutoa kwenye shule hiyo na kudai wapo viongozi wengi wa kitaifa waliosoma kwenye shule hiyo ambao hawajapata kuguswa na kuisaidia shule hiyo.
,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,mwisho,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,



















Post a Comment