WANAMICHEZO wanaoshiriki michezo mbalimbali,wameshauriliwa kuwa na
utaratibu wa kupima afya mara kwa mara ili kujiepusha na maradhi ambayo
yanaweza kuwatokea wawapo mchezoni ama baada ya michezo.
Ushauri
huo ulitolewa na Mganga Mfawidhi wa hospitali ya rufaa ya mkoa wa
Mara,Elias Godfrey,wakati akishiriki zoezi la kupima afya za wachezaji
wa klabu ya Biashara United,lililofanyika kwenye uwanja wa kumbukumbu ya
Karume mjini hapa.
Alisema suala la kuangalia afya kwa mchezaji
ni kitu muhimu kabla na baada ya kushiriki michezo na kudai kufanya
hivyo unakuwa umejiepusha na hatari ambayo inaweza kujitokeza ukiwa
kwenye mchezo husika.
Elias alisema kila mchezaji anapaswa
kuzingatia suala la kuangalia afya yake na sio vizuri kushiriki michezo
kwa muda mrefu bila kutenga muda wa kufanya vipimo na kujua maendeleo ya
afya.
"Niwashukuru sana uongozi wa klabu ya Biashara ambayo
imeamua kutenga muda wa kuangalia afya za wachezaji na hili ni jambo
kubwa ambalo linapaswa kuungwa mkono na kila mmoja.
"Tumewahi
kuwashuhudia baadhi ya wachezaji wakipata matatizo na wengine wakipoteza
maisha wakiwa mchezoni hivyo ni muhimu kuwa na utaratibu wa kupima afya
kwa kila mchezaji na ni vyema viongozi wa klabu nyingine wakawa na
utamaduni huu",alisema Elias.
Mganga huyo ambaye alikuwa
akishirikiana na wataalamu mbalimbali wa afya kupima na kutoa ushauri
kwa wachezaji hao,alisema ni vyema kila mchezaji aliyeshiriki zoezi hilo
kuzingatia ushauri waliopewa baada ya kufanyiwa vipimo.
Mwenyekiti
wa klabu ya Biashara United,Selemani Mataso,alisema kwa kujua umuhimu
wa kuangalia afya kwa wachezaji,waliamua kujipanga na kufanya zoezi hilo
huku akidi litakuwa endelevu kwenye klabu hiyo na kutoa wito kwa klabu
nyingine kuwa na utaratibu wa kuangalia afya za wachezaji.
LUZUNDANA AKIPATA USHAURI WA DOCTA BAADA YA VIPIMO
GEORGE AKIFATILIA MAELEZO YA DOCTA
KATOGORO HAKUWA NYUMA KUANGALIA AFYA
SHOMMI B BLOG PIA NI MMOJA WAO
SHUKU MMOJA WA MCHEZAJI KIONGOZI WA TIMU YA BIASHARA
FOLENI KWAAJILI YA VIPIMO
Home
»
»Unlabelled
» WACHEZAJI WA KLABU YA BIASHARA UNITED YA MUSOMA WAPIMWA AFYA ZAO
Post a Comment
0 comments