0

Mkuu wa Mkoa wa Mara, Kapten mstafu, Aseri Msangi, amewataka wananchi kuondokana na imani potofu kuwa upulizwaji wa dawa ya ukoko majumbani mwao kwa ajili ya kinga dhidi ya Malaria huchangia kupoteza nguvu za kiume.


Msangi ameyasema hayo juzi wakati akizindua zoezi la unyunyiziaji wa dawa ya koko lililofanyika katika wilaya ya Butiama  ambapo zoezi hilo litafanyika katika wilaya za Butiama na Musoma vijijini kuanzia machi 9 hadi April 22 mwaka huu ambapo jumla ya majengo 47,577 kwa Wilaya ya Butiama na 31,824 kwa Musoma vijijini zinatarajia kupulizia dawa ya ukoka.

Amesema imani potofu zimekuwa zikichangia kwa kiwango kikubwa kuzorotesha zoezi  hilo na kuwataka wanannchi kutoamini hivyo badala yake wawe tayari kushirikiana na wahusika pindi watakapokuwa wakiwafikia katika kaya zao.

Msangi amesema ugonjwa wa malaria mkoani Mara umekuwa tishio kwa asilimia 25 kutokana na taarifa ya utafiti wa viashiria vya Malaria na Ukimwi ulioendeshwa na Ofisi ya Taifa ya Takwimu na kudai juhudi zaidi zinapaswa zifanyike kati ya wananchi na taasisi mbalimbali ili kufikia kiwango cha kitaifa cha kupunguza malaria ambacho ni asilimia 9.

Hata hivyo amefafanua kuwa ugonjwa huo bado unaongoza kwa wagonjwa wengi wanaolazwa katika vituo vya afya na zahanati kwa nchi 10  za kusini mwa Afrika ikiwemo Tanzania ambapo nchi hizo zimekuwa zikichangia  takiribani asilimia 70 kwa ukubwa wa ugonjwa huo duniani.


Amesema kutokana na utafiti ina maana kwamba mtu mmoja anapoteza maisha kwa kila dakika moja kutokana na ugonjwa huo na kwa mwaka 2012 iliua watoto takiribani 482,000 wa umri chini ya miaka mitano na kudai ni jukumu la kila mmoja kutokomeza ugonjwa huo. 

Kwa upande wake Mkurugenzi wa shirika lisilo la kiserikali la Abt Associates  la Marekani ambao wanasaidia kutokomeza Malaria nchini Tanzania na Afrika kwa Ujumla,Dk. Nduka Uwuchukwu, amesema shirika hilo litaendelea kushirikiana na Tanzania katika kuhakikisha ugonjwa huo unapungua na kupunguza vifo vinavyotokana na ugonjwa huo.

Amesema jukumu la kupambana na Malaria ni la kila mmoja na ni muhimu kuhakikisha kila kaya inanyunyuziwa dawa ya ukoko ili kuteketeza mazalia yote ya mbu waenezao Malaria katika wilaya za Butiama na Musoma vijijini.

 MKUU WA MKOA AKIPOKELEWA NA KAMATI YA ULINZI NA USALAMA VIWANJA VYA OFISI YA HALIMASHAURI YA BUTIAMA
 TIMU YA WANYUNYUZIAJI
 MKUU WA MKOA AKITETA JAMBO NA DK.NDUKA ANAYEONGOZA TIMU YA WANYUNYUZIAJI KAMA M KURUGENZI WA SHIRIKA LA Abt
 MKURUGENZI WA Abt AKIZUNGUMZA WAKATI WA UZINDUZI
 MKUU WA MKOA AKIELEKEA KUZINDUA
 AKIPATA MAELEKEZO KABLA YA UZINDUZI
 AKIJIANDAA KUZINDUA


 BAADAE MAELEKEZO YALITOLEWA NYUMBA ZOTE ZINYUNYUZIWE

Post a Comment