0

MKUU wa wilaya ya Bunda, Lyidia Bupilipili, amezindua uandikishaji wa bima ya afya kwa watoto walio chini ya miaka 18 huku akitoa wito kwawazazi na walezi kuhakikisha wanatimiza wajbu wao kwa kuhakikisha kila anayelengwa anakatiwa ili aweze kupata huduma ya afya kwa uhakika.

Akizungumza kwenye uzinduzi huo uliofanyika kwenye kituo cha afya Bunda na kuhudhuliwa na wazazi,walezi na viongozi mbalimbali wakiwemo madiwani, alisema upo umuhimu mkubwa wa kuhakikisha kila mtoto anapata bima hiyo.

Amesema Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya (NHIF) umekuwa na malengo mazuri ya kuhakikisha inafikisha huduma bora za kiafya kwa wananchi kwa michango nafuu na huduma hii inayowalenga watoto ni wajibu wa kila mzazi na mlezi kuipa umuhimu wa pekee.

 Bupilipili amesema kiasi cha shilingi 50400 kinacholipwa kwa mwaka mmoja kwaajili ya kupata kadi ya mtoto aliye na umri chini ya miaka 18 itamsaidia kupata huduma hata pale mzazi anapokuwa hana pesa na kujiepusha na changamoto mbalimbali.

Amesema ugonjwa hauna taarifa na watoto wamekuwa wakiugua hivyo pale mzazi anapokuwa hana fedha kwa wakati anajikuta anaangaika kuomba fedha za kumtibia lakini anapokuwa na kadi ya bima anapata huduma mahali popote.
“ Wazazi na walezi tutimize wajibu wetu kwa kuhakikisha tunawakatia watoto wetu kadi za abima ya afya ili wawe na uhakika wa matibabu kwa wakati wowote na sio kusubili mtoto ameugua tunaanza kuomba fedha za matibabu kila mahala.

“ Niwashukuru pia Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya kwa kwa kuleta utaratibu huu kwa watoto wetu na kwa gharama nafuu kwa mwaka lakini ni vyema mkayaangalia na makundi mengine kwenye jamii”,amesema Bupilipili.

Meneja wa Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya mkoa wa Mara,Dk. Daud Zakaria Bunyinyiga, amesema uongozi wa wilaya ya Bunda umelipokea zoezi la uhamasishaji wa usaji wa watoto walio na umri chini ya miaka 18 kujiunga na bima ya afya na zoezi hilo limeanza vizuri.

Amesema mtoto anapokatiwa bima ya afya kwa gharama ya shilingi 50400 kwa mwaka anapata huduma kwenye hospitali,vituo vya afya na zahanati zaidi ya 700 nchini hivyo wazazi na walezi wapokee huduma hiyo kwa kuwa ina umuhimu mkubwa. 

Mzazi akiweka fomu baada ya kuandikishwa
 Burudani pia ilihusika kwenye uzinduzi

 Wanafunzi wakifatilia uzinduzi
 Meneja wa NHIF mkoa wa Mara,Dr.Daud Zakaria Bunyinyiga, akizungumza kwenye uzinduzi huo
 Mzazi akiandikishwa
Mkuu wa wilaya ya Bunda,Lyidia Bupilipili akizungumza kwenye uzinduzi huo
 Sister wa kituo cha yatima cha Mtakatifu Fransisko kilichopo Bunda akiwa na mmoja wa watoto wanaolelewa kwenye kituo hicho waliokatiwa kadi na mkuu wa wilaya

 Sister Anta Heshaj, akishukuru baada ya watoto wanaolelewa kwenye kituo cha Mtakatifu Fransisko kupewa kadi za afya na mkuu wa wilaya ya Bunda


Next
This is the most recent post.
Previous
Older Post

Post a Comment