0

  
   NA SHOMARI BINDA-MUSOMA

BENKI ya CRDB tawi la Musoma imeanza kutoa mikopo ya pikipiki ya magurudumu matatu(bajaj) pamoja na zile za magurudumu mawili kwa wajasiliamali vijana lengo likiwa ni kuwawezesha kiuchumi na kuondokana na umasikini.



Utaratibu wa benki hiyo umeanza kwa kuwawezesha wajasiliamali watatu kwa kuwakabidhi pikipiki 3 zenye thamani ya shilingi milioni 21 na kudai mikopo hiyo ni endelevu kwa wateja wake ambayo italipwa kwa zaidi ya mwaka mmoja.

Akizungumza mara baada ya kukabidhi pikipiki hizo, meneja wa benki ya CRDB tawi la MusomaWilfred Massawe, alisema wanaunga mkono juhudi za serikali katika kuwaondolea umasikini watanzania na mikopo hiyo waliyoitoa ikitumiwa vizuri itainua kipato cha familia.


Alisema kabla ya wahusika kukabidhiwa mikopo hiyo ya pikipiki za miguu mitatu wahusika walipewa elimu ya matumizi mazuri na namna ya kufanya biashara hiyo ya usafirishaji na iwapo watazingatia mradi huo utawatoa sehemu moja kwenda nyingine.

Massawe alisema mikopo hiyo ina tija na lengo lake ni kuinua uchumi wa wateja wake na wananchi huku marejesho yake yakiwa ya muda mrefu na kusisitiza matunzo mazuri ya pikipiki hizo ili malengo yake yaweze kutimia.


“ Tumekabidhi pikipiki hizi za magurudumu matatu kwa wateja wetu kama mkopo kwaajili ya kuongeza kipato chao na mikopo hii ni endelevu tukiunga mkono juhudi za serikali katika kuinua kipato cha wananchi”,alisema Massawe.

Meneja wa biashara wa benki hiyo tawi la Musoma, Muzi Naugali, alisema biashara hiyo ya usafirishaji iwapo itatumiwa vizuri na wahusika itawanufaisha na hata kuongeza biashara nyingine kutokana na pikipiki hizo.


Kwa upande wake meneja mikopo wa benki hiyo, Alexander Reuben, alisema elimu juu ya matumizi bora ya mikopo wameitoa na kuwa na imani wahusika wataitumia kufanya marejesho na kuyakamilisha hatimaye kuzimiliki pikipiki hizo.


Wateja waliopokea pikipiki hizo wameishukuru benki ya CRDB kwa utaratibu huo waliouanzisha ambao utawasaidia kuwaongezea kipato na kuahidi kuutumia mkopo huo vizuri ili uweze kuwainua kiuchumi












Post a Comment