0
KAMANDA WA JESHI LA POLISI MKOANI MARA ABSALOM MWAKYOMA AKIWAOMBA RADHI WAANDISHI WA HABARI NA KUONDOA TOFAUTI ILI WAENDELEE KUANDIKA HABARI ZA JESHI HILO
WAANDISHI WA HABARI WAKIMSIKILIZA MWENYEKITI WA CHAMA CHA WAANDISHI WA HABARI MKOANI MARA EMANUEL BWIMBO AKIWASII WAANDISHI WAPITISHE MAAMUZI YA KUONDOA TOFAUTI NA JESHI LA POLISI KATIKA UKUMBI WA UWEKEZAJI WA MKOA WA MARA
KATIBU TAWALA WA MKOA WA MARA CLEMENTI LUJAJI AKIZUNGUMZA JAMBO HUKU AKIKISISITIZA UMUHIMU WA WAANDISHI WA HABARI
MWENYEKITI WA MRPC EMANUEL BWIMBO AKIZUNGUMZA JAMBO KULIA NI OFISA PROGRAM MWANDAMIZI WA BARAZA LA HABARI TANZANIA MR BANZI ALIYESIMAMIA MKUTANO WA WAANDISHI NA WADAU WA HABARI MKOA WA MARA KUTOKA MAKAO MAKUU JIJINI DAR ES SALAM
MWENYEWE NILIKUWA MAKINI ZAIDI KATIKA MKUTANO HUO NIKIWA PEMBENI NA MRATIBU WA ASASI YA MARA DEVELOPMENT FORAM GEORGE CHIBASA
WAANDISHI WA HABARI WAKIPIGA KURA ZA MIKONO KUMALIZA TOFAUTI NA JESHI LA POLISI MKOANI Na Shomari Binda
        Musoma,

Waandishi wa Habari Mkoani Mara wameamua kumaliza tofati zao na Jeshi la Polisi baada ya kuweka mgomo wa kuandika Habari kutoka katika Jeshi hilo tangu Septemba 11 Mwaka huu baada ya kuzuia maandamano ya kupinga kifo cha mwana habari Daudi Mwangosi.

Maamuzi ya Kusitisha mgomo huo umetolewa leo kwa kauli moja na Chama cha Waandishi wa Habari Mkoani humo katika mkutano na wadau wa Habari uliofanyika katika ukumbi wa uwekezaji wa Mkoa wa Mara.


Kamanda wa polisi mkoani Mara kamishina mwandamizi   wa jeshi la polisi Abslom Mwakyoma kupitia mkutano huo amewaomba radhi waandishi wa Habari kwa tofauti zilizojitokeza na kusema kuwa Jeshi hilo linawategemea sana waandishi wa Habari katika kufikisha tofaoti mbalimbali katika jamii.

Alisema kama ni adhabu waliyotoa Waandishi wa Habari kwa Jeshi la Polisi tangu Septemba 11 wamejifunza na kudai kuwa watahakikisha tofauti zilizokuwepo zinamalizika na kufanya kazi kama timu katika kuisaidia jamii.

Alisema hivi sasa kumeibuka makundi ya wahalifu ya Mbio za vijiti,Mdomo wa furu,Jamaica mocas na G5 ambayo yametishia amani kwa wananchi wa Manispaa ya Musoma na wakati mwingine kusababisha mauji ya raia, hivyo alisema jeshi hilo limejipanga kukabiliana na makundi hayo kuanzia sasa na kueleza bila ushirikiano na Waandishi wa Habari hawawezi kufanikisha.

Kuhusu hatua ya waandishi wa habari mkoani Mara kususia kuandika habari za jeshi la polisi kutokana na kuzuiwa kwa maandamano  hayo,kamanda Mwakyoma,alisema hatua hiyo ilichukuliwa baada ya kubaini kuwa maandamano hayo hayakufuata taratibu za sheria.



Awali katibu tawala mkoa wa Mara Bw Clement Lujaji,akizungumza wakati akifungua mkutano huo,amewaomba waandishi wa habari mkoani Mara kufanya kazi kwa kuzingatia uzalendo pamoja na kuibua fursa zitakazo lenga kuchochea ukuaji wa uchumi wa wananchi  wa mkoa wa Mara.
Alitumia nafasi hiyo,kuliomba jeshi la polisi na waandishi wa habari mkoani Mara,kuondoa tofauti zao ambazo zilijitokeza na kusababisha kususiwa kuandikwa kwa habari za jeshi hilo na hivyo kuwanyima haki wananchi kupata habari ambao ni haki yao ya msingi.

Kwa sababu hiyo waandishi wa habari wa mkoa wa Mara kwa kauli moja chini ya uenyekiti wake Bw Emanuel Bwimbo,walitangaza kuondoa mgomo wa kuandika habari za jeshi la polisi kuanzia sasa na kwamba wamemtaka kamanda wa polisi kukemea unyanyasaji ambao umekuwa ukifanywa na askari wake dhidi ya waandishi mkoani Mara.
 




Post a Comment