0
NI MKAO WA KIMIJADALA ZAIDI KATIKA WARSHA

WASHIRIKI WA WARSHA WAKIJADILIANA

NI VIJIMAMBO VYA KUTOA UCHUVU BAADA YA KUKAA SANA KWENYE WARSHA




MWENYEKITI WA WARSHA NYARUGENDA MKURUGENZI WA ABC FOUNDATION

WATU WANATOA MTAZAMO WAO


NAMI SIKUWA MBALI KATIKA KUJADILIANA NA WENZANGU

Na Shomari Binda
       Musoma,

Wanaharakati wa asasi mbalimbali za Utetezi wa haki za Binadamu Mkoani Mara wametakiwa kuendeleza harakati zao kwa kupigia kelele Sheria ambazo zimepitwa na wakati na kuendelea kumkandamiza Mwanake hapa Nchini.

Wito huo ulitolewa na muweseshaji wa Warsha ya mafunzo kwa watoa msaada wa Kisheria na Watetezi wa Haki za Binadamu juu ya uelewa kuhusu Haki Kisheria za Wanawake ,Desdevia Haule iliyoandaliwa na Shirika la Wanawake katika Sheria na Maendeleo Barani Afrika (WiLDAF) iliyofanyika katika ukumbi wa mikutano wa Kanisa la Anglican Mjini Musoma.

Alisema zipo Sheria ambazo moja kwa moja zinamkandamiza Mwanamke ikiwemo Sheria ya Mirathi ambapo kwa kiasi kikubwa zinawanyanyasa Wajane na Watoto wa kike huku Sheria za Kilmila zikiwa hazimtambui Mjane kama Mrithi wa moja kwa moja.

Alidai katika Sheria hiyo Mjane Hurithi kupitia Watoto wake na pia kanuni katika Sheria hiyo zinamchukulia Mtoto wa kike kama mtu wa saraja la tatu baada ya Mtoto wa kiume huku Mtoto wa kiume akiwekwa katika daraja la kwanza.

Mwezeshaji huyo aliongeza kuwa mkataba wa nyongeza wa Haki za Wanawake Barani Afrika wa Mwaka 2003 ambapo Tanzania iliridhia mkataba huo mnamo Mwaka 2007 na kukubali kama Nchi kubanwa na masharti yaliyomo lakini bado haki hizo hazitekelezwi.

Alisema katika mkataba wa Kimataifa wa kuondoa aina zote za ubaguzi dhidi ya Wanawake wa Mwaka 1979 ulioazimiwa na Umoja wa Mataifa Tanzania ni sehemu ya utekelezaji wa mkataba huo.

"Baasdhi ya Haki ambazo zimetakwa katika Mkataba huu na kuagiza Nchi husika kuhakikisha kuwa hakuna ubaguzi dhidi ya Wanawake ni pamoja na haki ya kupiga kura (Ibara ya 7),Utaifa (Ibara ya 9),(Elimu) ibara ya 10)Ajira (Ibara ya 11),Afya (Ibara ya 12),Uchumi (Ibara ya 13 pamoja na Ndoa (Ibara ya 16),"alisema mwezeshaji huyo.

Akizungumzia suala la ukeketaji kwa Wanawake,Desdevia ambaye kitaaluma ni Mwanasheria alisema jambo hilo ni udhalilishaji wa Mwanamke na kumshushia hadhi yake hivyo kila Mwanaharakati anapaswa kupambana nalo na kuhakikisha linakomeshwa Mkoani Mara.

Washiriki wa Warsha hiyo inayofanyika kwa siku tatu itakuwa na mada mbalimbali ikiwemo Mikataba na Maazimio ya Kimataifa kuhusu Haki za Binadamu za Wanawake,Sheria ya Ndoa ya Mwaka 1971 pamoja na Sheria ya Aridhi Sura Na.113 na 114 za Mwaka 1999
 



Post a Comment