0
  Suala la watu kutekwa na kukatwa vichwa laingia hatua nyingine

     -Aliyetekwa na kufanya kazi ya kupakia vichwa asimulia kila kitu

Mbunge Nyerere ataka askari walipwe

Na Shomari Binda
         Musoma,

SUALA la watu kutekwa na kukatwa vichwa limechukua sula nyingine baada ya mtu mmoja aliyefahamika kwa jina la Obwanga Jamara mkazi wa Utengi eneo la Ingili chini katika Wilaya ya Rorya kutekwa na watu wasiofahamika na kuamuliwa kupaki vichwa vya Binadamu katika visado vya rangi.

Akizungumzia kisa cha kutekwa alipokuwa akizungumza na BLOG HII katika Hospitali ya Mkoa wa Mara alikokuwa amelazwa katika chumba cha ICU kutokana na maumivu makubwa aliyoyapata kutokana kwa watekaji alielezea kila kitu huku akilishitumu Jehi la Polisi kwa kushindwa kufatilia.

Alisema alifika katika Kijiji cha Nyankanga akitokea nyumbani kwake Utegi kwa lengo la kukata mti wake wa mbao uliopo kijiji hapo Desema 27 na ndipo alipokutana na dhahama ya kutekwa na kushuhudia maovu makubwa yanayofanywa na watekaji hao.

Alisimulia kuwa alipokuwa katika maeneo hayo alikuwa katika maeneo hayo akiwa anatafuta mashine ya kupasulia mbao ambapo huo ulikuwa mti wake wa pili kwenda kuukata na mashine aliipata hapohapo kijijini kwa kukodi.

“Nilifika Nyankanga nikiwa natafuta mashine baada ya mtu wa kwanza aliyenikodishia kumkosa na kuanza kuulizia ndipo nilipokutana na vijana wawili ambao walidai wanamfahamu mtu ambaye anayo mashine.

“Nilichukuliwa na vijana hao na kufika mbele kidogo tulipanda kwenye gari inayodaiwa ndio iliyokuwa ya mtu anayedaiwa kuwa na mashine ili kwenda kuufata nyumbani kwake na kufika njiani niligeuziwa kibao.

“Nikiwa nimewekwa katikati na wale vijana wawili nilitolewa mfano wa bastora nilipoiona niligundua sio halisi pamoja na sime na kuambiwa nitoe pesa na mfuko wa ndani nilikuwa na shilingi elfu sitini nikatoa na kuwapa,”alieleza.

Alisema baada ya kutoa pesa hizo alifunikwa uso wake kwa shati lake alilokuwa amevaa na kuwekwa nyuma ya buti ya gari na kupelekwa mahala kukojulikana ambako alikutana na ukatili mkubwa unaofanywa na watekaji hao.

“Baada ya kuzungushwa sana huku nikiwa nyuma ya buti ya gari niliingizwa ndani ya nyumba ambayo siwezi kuifahamu na kuachwa humo na wenyewe kuondoka huku nikiwa bado nimefungwa macho na kusikia sauti ya kike ikilia ndani ya nyumba hiyo.

“Baada ya muda kupita watu wale walirejea na kunivua kitambaa machoni na kuniwekea box mbele na kuniamulu nifungue na kukutana na vichwa vitatu vya Binadamu na nilivyoviona ni vya watoto kati ya miaka mitatu ama mitano.

“Huwezi kuamini ndugu Mwandishi ni hatari na Serikali isipo fatilia jambo hili hali itakuwa mbaya sana maana suala hili lipo na mimi nimelifanya kwa mikono yangu mwenyewe baada ya kutekwa.

“Nilivitoa vile vichwa kwenye box nikishirikiana na Yule dada niliyemkuta mle ndani nakuambiwa niviweke kwenye kisado cha rangi kimoja baada ya kimoja na kisha kuweka udongo wa mfinyanzi huku jua tukiweka rangi na kufunga,”aliendelea kusimulia muhanga huyo.

Alisema baada ya kumaliza kufanya kazi hiyo aliyoamuliwa na watu waliomteka walimfunga tena kitambaa machoni na kumtoa ndani ya nyumba na kumpakia nyuma ya buti ya gari na kumpleka kusiko julikana.

“Tukiwa njiani huku mimi nikiwa nyuma ya buti ya gari ilisimama na wale watu kushuka na kuanza kuisukuma……inaonekana ilizimika lakini nilisikia watu wakipita barabarani nakusalimiana habari afande July,”aliendelea kusimulia.

Alisema baada ya gari kushindwa kuwaka na watu waliokuwa wakisalimiana nao kupita aliwasikia watu hao wakipiga simu kuomba gari lingine na kuambiwa kuwa halipo waangalie wafanyeje.

“Baada ya gari kushindwa kuwaka walinishusha kwenye gari huku nikiwa bado nimefunikwa macho na kupelekwa mahala na kutupwa huku mmoja wao akisema mmalizie kabisa ambapo walinikanyaga kifuani na kichwani na kupoteza fahamu na kujua kuwa tayari wameshaniua,”aliongeza.
 
         KUOKOTWA NA POLISI MAKABURINI

Obwanga alisema baada ya kupata nafuu katika chumba cha wagonjwa mahututi alisimuliwa na wauguzi hospitali hapo kuwa alifikishwa na askari Polisi na kudaiwa ameokotwa katika makaburi ya Menonite katika Manispaa ya Musoma Desemba 28.
Anadai baada ya kufikishwa Hospitalini hapo hakuna askari yeyote aliyefika kwa muda kumchukua maelezo ili wale waliofanya tukio hilo waweze kufatiliwa lakini haikuwa hivyo.

“Hadi jana (juzi) Desemba 30 saa mbili usiku ndipo nilipoona askari wanakuja kunichukua maelezo nilitaka kugoma lakini nikaamua kutoa kutokana na kushauliwa na wauguzi baada ya kuwaona Polisi hawatimizi majukumu yao kwa wakati,”alisema.
   
  MEYA AZUNGUMZA NA KAMANDA

Baada ya kukutana na muhanga huyo kutokana na taarifa za Mwandishi wa Habari hizi,Meya wa Manispaa ya Musoma Alex Kisurura (Chadema) alikutana na Kamanda wa Jeshi la Polisi Mkoani Mara Absalom Mwakyoma akiwa na muhanga  na kukili kupokea tukio hilo na kuahidi kulifanyia kazi kwa kina.

"Tumeongea na Kamanda wa Polisi wa Mkoa na kutuhakikishia suala hilo linafanyiwa kazi kwa nguvu zote na Jeshi na kuahidi kutoa matokeo yake baada ya kukamilisha shughuli nzima,"alisema Meya Kisurura.  

   NYERERE ATAKA POLISI WALIPWE

Akizungumza kwa njia ya simu na Blog  hii Mbunge wa Jimbo la Musoma Mjini Vicenti Nyerere alisema kitendo cha askari Polisi kutokachukua hatua za haraka ni kutokana na baadhi yao kutolipwa mafao yao kwa wakati na kufanya kazi katika mazingira magumu.

Alisema zaidi ya askari 230 Mkoani Mara wanadai fedha zao hali inayopelekea kutokuwa na moyo wa kufanya kazi kwa ufanisi na kupelekea kutokea kwa matukio mbalimbali ambayo yanaweza kukabiliwa. 

Post a Comment