0
    Profesa Muhongo aijibu CUF kuhusu mgawo wa umeme

    Na Shomari Binda,
         Musoma


WAZIRI wa Nishati na Madini Profesa Sospeter Muhongo amesisitiza kuwa hakuna hoja ya mgawo wa umeme kwa sasa hapa Nchini kutokana na Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO) kujipanga kutafuta vyanzo vingine vya uzalisha mbadala wa umeme kuliko kutegemea maji ili ifikapo Mwaka 2013 Tanzania iweze kupata umeme wa uhakika.

Kauli hiyo ameitoa Mjini hapa katika kikao kilichowashilikisha Vijana wa Manispaa ya Musoma kutaka kujua ni changamoto gani zinazopelekea Mji huo kukosa Maendeleo na kuzungummzia jinsi Shirika hilo linavyoendeleaa kufanya mabadiliko katika maeneo mbalimbali ya kiutendaji ili kuweza kufanya kazi kwa ufanisi na kupata umeme wa uhakika.

Alisema anapingana na maazimio yaliyotolewa na Chama cha Wananchi (CUF) katika Baraza lake Uongozi lilofanyika hivi karibuni Jijini Dar es salaam na kueleza kuwa upo mgawo usio rasmi wa umeme ambao unapelekea kero kwa Wananchi na kukwamisha shughuli za kimaendeleo ambazo zinahitaji nishati ya umeme.

Profesa Muhongo alisema suala la kukatika kwa umeme kwa dakika mbili ama tatu sio mgawo kama inavyoelezwa na Chama hicho bali ni kutokana na miundombinu ambayo imechakaa ambapo kwa sasa Tanesco imeelekeza katika kufanya jitihada za kuibadilisha ili kuweza kukabiliana na changamoto hiyo.

''Sote tunafahamu miundombinu ya Shirika hili mingi imechakaa na inahitaji mabadiliko ambayo kwa sasa kwa asilimia kubwa inafanyiwa kazi hivyo inapelekea kuwepo na kero ya kukatika kwa umeme kwa muda furani lakini sio kila siku na huo sio mgawo wa umeme jamani tuache propaganda za kisiasa katika masuala mengine ya maslahi ya Taifa,"alisema Muhongo.

Alisema yeye akiwa kama Waziri mwenye dhamana ya umeme atamueleza Waziri Mkuu ama Rais iwapo kutakuwa na mgawo wa umeme lakini sio watu kusimama na kusema kuna mgawo kitu ambacho amekiita ni uzushi ambao unatumiwa na wanasiasa katika propoganda zao ambazo hazina tija kwa Taifa.

Alidai Tanesco inajipanga kuhakikisha umeme wa uhakika unapatikana na tayari imeanza programu ya kusambaza umeme Nchi nzima katika Vijiji na Wilaya na kusema kazi hiyo inahitaji kupana ushirikiano katika kuifanukisha na kuomba kupata maoni kwa kila Mwananchi namna ambavyo anataka shirika hilo lifanye katika kuleta ufanisi tofauti na kipindi cha nyuma

Aidha Profesa Muhongo alisema zipo changamoto nyingine ambazo zinafanywa na watu wasio wazalendo kwa kuiba mafuta ya Transifoma pamoja na waya za umeme hali inayopelekea kujitokeza kwa matatizo ya kukatika kwa umeme ili kupisha mafundi kuweza kurekebisha na kurudisha umeme na kuwaomba Wananchi kuweza kutoa taarifa pale wanapoona mtu anataka kuhujumu shirika hilo.

Akizungumzia masuala ya kimaendeleo katika Mji wa Musoma,Waziri Muhongo aliwataka vijana wa Mji huo kuacha ubinafsi na kushirikiana katika kujitafutia Maendeleo na kubadilisha muonekano wa Mji huo na kusisitiza kujiepusha na kukalia siasa muda wote bali wajishughulishe na shughuli mbalimbali za kujiletea maendeleo.

Post a Comment