0

Na Shomari Binda
     Musoma,

HOSPITALI ya mkoa wa Mara iko katika hatari kubwa ya kukubwa na milipuko ya magonjwa mbalimbali yakiwezo ya kuhara kutokana na wodi zake nyingi kukosa vyoo jambo ambalo linasababisha wagonjwa kujistili  ovyo ndani na nje ya wodi hizo.

Mwandishi wa habari hizi juzi alishuhudia kinyesi kingi kikiwa kimetapakaa nje ya wodi hizo huku wagonjwa wakitumia vyombo kama madishi na majagi kwaajili ya kuhifadhia mkojo.

Baadhi ya watu ambao wanaguza ndugu zao katika wodi namba saba na tatu katika hospitali hiyo,waliliambia gazeti hili kuwa wagonjwa wanalazimika kujisitili nje ya wodi hizo na kusababisha kutapakaa ovyo  kwa kinyesi hicho.

Walisema hivi sasa wanalazimika kununua vyombo kama madishi na majagi kwaajili ya kuhifadhi mkojo  wa waguzi wa wagonjwa na wagonjwa hasa nyakati jambo ambalo walisema linaweza kusababisha milipuko mikubwa  ya magonjwa endapo hatua za haraka hazitachukuliwa kukabili hali hiyo.

“Wewe ona uwanja wote huu umejaa kinyesi hayo madishi uliyaona humu ndani si kwamba yamehifadhi maji bali ni mkojo kwani wodi hii na zingine zote hazina vyoo”alisema mama mmoja juzi usiku wakati akizungumza naBLOG HII .

“Sehemu hii ambayo unaona kuna marundo marundo ya mchanga hicho ni kinyesi kimefukiwa na watu asbihi wanakaa katika maeneo haya hivi unategemea nini kama si magonjwa…kweli sehemu ya afya kama hii hali inakuwa hivi je hapa tunajifunza nini sisi”alihoji mzee Ramadhan Said.

Mganga mfawidhi wa hospitali hiyo ya mkoa wa Mara Dk Iragi Ngerageza akizungumzia suala hilo kwa njia ya simu alikiri wodi hizo kukosa vyoo kwa madai kuwa majengo hayo ni ya muda mrefu na kwamba tayari mhandisi wa ujenzi wa mkoa ameombwa kuandaa michoro mipya ya kuwezesha ujenzi wa mfumo mzima wa maji machafu na vyoo hivyo.

“Ni kweli kabisa hayo unayouliza ndio yapo katika hospitali hii,kama unavyojua mimi ni mgeni nimekuja juzi nilipokuta hali hii nilitishika sana sana hivyo ilinibidi kumwite mhandisi wa mkoa kwaajili ya kuona hatua za haraka za kuchukua ikiwa ni pamoja na kuandaa michoro ya kuwezesha kujenga mfumo mzima wa maji machafu na vyoo hivyo kwani majengo haya ni ya muda mrefu”alisema mganga huyo mfawidhi.

Hata hivyo alisema baada ya waziri wa Afya na Usatawi wa jamii kuteua wajumbe wa bodi ya uendeshaji wa hospitali hiyo ambayo inatarajiwa kuzinduliwa kesho,itasadia kwa kiasi kikubwa kutatua changamoto nyingi zinazoikabili hospitali hiyo hivi sasa.

Post a Comment