1
Jeshi la Mali limesema kuwa litachunguza madai kuwa wanajeshi wamewaua raia wasio na hatia katika eneo linalodhibitiwa na wapiganaji wa kiisilamu la Kaskazini

 Afisaa mkuu wa jeshi alisema  kuwa kwa sasa hawezi kuthibitisha au kukanusha   kuwa mauaji yalifanyika.
Shirikisho la kimataifa la kutetea haki za binadamu hapo jana lilituhumu wanajeshi wa Mali kwa kuwaua waarabu na watu wa jamii ya Tuareg ambao ni wachache.

Kwingineko, moja ya makundi ya wapiganaji wa kiisilamu Kaskazini mwa Mali, limegawanyika na kusema linataka kufanya mazungumzo.

   kwa mujibu wa taarifa za shirika la habari la AFP lililoweza kutupia jicho taarifa ya wapiganaji hao.

Vuguvu la (Islamic Movement for Azawad,) lilisema kuwa linajitenga na kundi zima la Ansar Dine, na linapinga vitendo vyote nvya kigaidi au siasa kali.

Kulingana na taarifa hiyo, kundi hilo linaongozwa na Alghabass Ag Intalla, kiongozi muhimu katika eneo la Kidal. Kidal.

Ufaransa ilituma kikosi cha jeshi, mapema mwezi huu ili kujaribu kukomesha harakati za makundi hayo.

Ilisema kuwa baadhi ya wapigananaji wenye uhusiano na kundi la al-Qaeda, na baadhi yao wakiwa wageni, walitishia kugeuza Mali kuwa taifa la kigaidi.

Na katika harakati zinazoendelea dhidi ya wapiganaji wa kiisilamu, mapema leo,watetezi wa haki za bibadamum, wamedai kuwa jeshi la Mali limewaua “kiholela watu kadhaa” katika harakati za kujaribu kuteka tena eneo la kaskazini lililoko chini ya mamlaka ya wapiganaji wa Waisilamu.

Shirikisho la Kimataifa la Kutetea Haki za Binadamu, FIDH, limesema kwamba watu kadhaa waliuwawa kwa ajili tu walikuwa hawana vitambulisho.

Lakini mwanajeshi mmoja wa Mali alinukuliwa akikanusha madai hayo.
Madai mengine kuhusu mauaji ya kiholela pia yameripotiwa katika maeneo mengine ya magharibi na kati mwa nchi hiyo.
Kiongozi wa kundi la wapiganaji wa Ansar Dine

Habari zinazosema kwamba jeshi hilo, ambalo wengi wao ni Waafrika weusi kutoka kusini mwa nchi, wamekuwa wakiwalenga Waarabu na Watuareg kutoka kaskazini, jambo linaloashiria ubaguzi wa rangi katika mapigano hayo, ubaguzi ambao umefichwa na kuwepo kwa vikosi kutoka nchi za magharibi wanaopambana na wanamgambo Kiisilamu.

chanzo BBC

Post a Comment

This Site tramadol hcl monograph - tramadol hcl and weed