Musoma,
Mkuu wa Wilaya ya
Musoma Jackson Msome amewafagilia Madiwani wa Halimashauri ya Wilaya ya Musoma
ambao wegi wao wanatokana na Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) kwa
kuwa mstari wa mbele kusimamia maslahi ya Umma ikiwemo mahindi ya chakula cha
bei nafuu yaliyotolewa na Serikali.
Msome alitoa kauli
hiyo alipokuwa akihitimisha juma la kisomo la elimu ya watu wazima katika
ukumbi wa Chuo cha Maendeleo ya Jamii Buhare na kusema kitendo cha uwajibikaji
katika shughuli za kimaendeleo zinapaswa kuungwa mkono.
Alisema katika
kufatilia chakula cha bei nafuu kilichotolewa na Serikali katika kukabiliana na
njaa Madiwani hao wamekuwa mstari wa mbele katika kuhakikisha Manispaa ya
Musoma ambayo imedaiwa kuwa na njaa kubwa inapata chakula cha kutosha.
Msome alisema
Madiwani wote wamekuwa kitu kimoja katika kulifatilia suala hilo na kuhakikisha
Manispaa ya Musoma inapata tani 400 kati ya 900 za mahindi zilizotolewa na
Serikali kutoka ghala la Taifa la kuhifadhi chakula Mkoani Shinyanga kuja Mara
katika kukabiliana na uhaba wa chakula.
“Katika suala hili
Madiwani wameweka itikadi zao pembeni za kisiasa na kushiliki kikamilifu katika
kuhakikisha mahindi ya chakula kilichotolewa na Serikali knafika kwa wakati na
Wananchi wanapata kutokana na bei elekezi iliyotolewa na Serikali,”alisema
Msome.
Alisema tayari
mahindi ya chakula katika kukabiliana na njaa yameanza kuingizwa katika
Manispaa ya Musoma kutoka kwa wafanyabiashara walioteuliwa na kuuzwa kwa bei
elekezi ya Serikali ambapo kilo moja ya mahindi inauzwa kwa bei ya shilingi 700
huku kilo moja ya unga wa sembe ikiuzwa kwa shilingi 900.
Mkuu huyo wa Wilaya
aliwataka Madiwani wa Manispaa ya Musoma kuendelea kutoa ushirikiano katika
kufatilia uuzwaji wa mahindi hayo ili Wananchi wasije kuuziwa kwa bei zaidi
kutoka kwa wafanyabiashara ambao wameteuliwa.
“Kunaweza kutokea
wafanyabiahara wasio waaminifu ambao wanaweza kuwauzia Wananchi mahindi haya
kwa bei ya juu naomba tuwe kitu kimoja katika kilifatilia hili ili bei halisi
iliyopangwa iweze kutumika katika kuyauza,alisema Msome.
Aidha Mkuu huyo wa
Wilaya aliwataka pia Wananchi kutoa ushirikiano kwa viongozi pale watakapoona
wafanyabiashara wanauza mahindi hayo kwa bei ya juu ili waweze kuchukuliwa
hatua kutokana na bei hiyo kupangwa na wafanyabiashara walioteuliwa kukubaliana
kufata katika ghala la Taifa la kuhifadhi chakula na kuuza kwa bei elekezi.
Kwa
upande wake Diwani wa Kata ya Buhare Lucas Katikilo (CHADEMA) ambaye
alikuwa pamoja na Mkuu huyo wa Wilaya katika hitimisho la juma la kisomo
alisema watazingatia wito wa Mkuu wa Wilaya katika kufatilia uuzwaji wa
mahindi hayo kwa bei elekezi iliyopangwa na Serikali.
Post a Comment
0 comments