0
Na Shomari Binda
          Musoma,

KUPANDA kwa bei ya nyama  mara kwa mara  katika Manispaa ya Musoma kumepelekea kuwatanisha  viongozi wa Halmashauri  ya Manispaa pamoja na Wafanyabiashara wa nyama  baada ya malalamiko  kutoka kwa wananchi.

Katika kikao hicho kilchofanyika  katika ofisi ya Meya wa Manispaa ya Musoma  hoja ya malalamiko  ya Wananchi na kupelekea  kikao  hicho ni bei ya nyama  kutoka shilingi elfu 4000 hadi 5000 ,huku bei  ya nyuma  ikiwa kati y ash 2500 hadi 3000 kwa kilo ya nyama.

Zaidi ya malalamiko ya Wananchi ni kutokana na madai ya kuwepo  kwa idadi  kubwa  ya ng’ombe  katika  Mkoa wa Mara  tofauti na mikoa mingine  na badala yake  bei imekuwa  ikipanda  mara kwa mara na kuleta kero .

Kwa upande wao wafanyabiashara wa nyama katika manispaa ya musoma  wamesema kuwa bei yao ni halali kutokana na kupanda kwa ng’ombe  katika minada  kutokana na ushindani  unaopatikana katika minada.

Mmoja wa wafanyabiashara  Joseph Magita  amesema kuwa  wanunuzi wa ng’ombe  minadani  kutoka nchi jirani ya Kenya  wamekuwa wakiharibu soko la ng’ombe  minadani  kwa kupandisha bei  ambapo inafika wakati ng’ombe mmoja ananunuliwa hadi shilingi milioni moja na nusu.

‘’ Vipi tutaendelea kufanya  biashara  ya hasara kwa maana zaidi ya milioni moja kwa ng’ombe  huwezi kununua na kuuza shilingi elfu 3000  kwa kilo  lazima tuangalie kipindi cha soko ‘’alisema  Magita.

Hata hivyo hoja za wafanyabiashara  hao kuhusiana na ushindani wa bei minadani  zilikinzana na viongozi  pamoja na madiwani waliokuwepo katika kikao hicho  kwa madai soko la nyama  katika wilaya  nyingine za mkoa wa mara ambao wananunua katika soko moja  na ipo chini.

Diwani wa Kata ya Makoko (CHADEMA)  na Mwenyekiti wa Kamati ya Huduma za Jamii Aloyce Mawazo alisema wafanyabiashara  wa nyama  katika Manispaa ya Musoma  lazima waliangalie suala  la bei  ili kuendana na soko  la ulaji  wa nyama.

Kwa upande wake Meya wa Manispaa ya Musoma Alex Kisurura (CHADEMA) aliwashauri wafanyabiashara hao kuto kuangalia kutaka faida kubwa katika biashara bali waangalie mzunguko wa kibiashara ambao wanaufanya katika soko kutokana na muitikio wa walaji.

Alisema kwa sasa walaji wengi wameshindwa kununua nyama kutokana na kupanda kwa bei hali inayosababisha kulala kwa nyama katika mabucha kwa zaidi ya siku mbili na kuwakosesha mapato.

"Natambua mpo katika soko hulia lakini lazima muungalie mzunguko wa kibiashara wa nyuma na kipindi hiki ambacho mmepandisha bei...watu wengi hawanunui nyama na sindhani kama itakuwa na faida kwenu na tumewaita hapa kupeana ushauri na sio kuwapangia bei,"alisema Kisurura.

Katika hatua nyingine Meya huyo wa Manispaa ya Musoma amesema wapo katika mabolesho makubwa katika machinjio ya nyama na bucha ili kuweka mahala salama pa kuchinjia na kuuzia nyama.

Alisema Manispaa ya Musoma imetenga shilingi milioni 9 zikilenga kufanya ukarabati katika bucha za soko kuu la Musoma ikiwa ni pamoja na kuwekea nishati ya umeme na ukarabati wa jengo.

Post a Comment