0
WAPIGANAJI WA M23
Waasi wa kundi la M23 katika Jamuhiri ya Kidemokrasia ya Congo, wametangaza kusitisha vita kabla ya awamu ya pili ya mazungumzo ya amani na serikali.

Katika mkutano na waandishi wa habari mjini Kampala, Uganda, waasi hao walisema kuwa wanatumai serikali nayo itafanya vivyo hivyo.
Jaribio la mwezi jana la kutafuta mwafaka, wa kumaliza vita vya miezi tisa mashariki mwa DRC liligonga mwamba.

Hadi watu laki nane, wameachwa bila makao tangu waasi walipoanza mapigano dhidi ya serikali mwezi Mei.

"sisi daima tumekuwa tukitaka amani. Leo, tunatangaza kuwa tumesitisha vita'' alisema msemaji wa kundi hilo, Francois Rucogoza.

"hata kama serikali itakataa kutia saini makubaliano ya amani, tutaendelea na mazungumzo'' aliongeza kusema bwana Rucogoza.

 Waasi wa M23, wameituhumu serikali ya rais Joseph Kabila kwa kukosa kutii mkataba wa awali wa amani, kuweza kuwajumuisha waasi hao katika jeshi la serikali.

Post a Comment