0

BAADHI YA WANAWAKE WAKIWA KATIKA UWAJIBIKAJI SEHEMU ZA MIGODINI
                              

Na Shomari Binda
        Butiama,
MWENYEKITI wa Jumuiya ya Wanawake wa CCM Wilaya ya Butiama (UWT) na Diwani wa Kata ya Bwiregi Nyagheti Adam alisema katika ziara yake ya kuwashukuru Wananchi wa Wilaya ya Butiama kwa kumchagua kuwa Mwenyekiti wao atakayoianza hivi karibuni moja ya mambo  atakayofanya ni kuwahimiza Wanawake kujikita katika shughuli za Ujasiliamali.
Akizungumza na Waandishi wa Habari katika Ofisi za UWT,Nyagheti alisema katika ziara hiyo ambayo atazunguka katika kata zote za Wilaya ya Butiama akiambatana na walimu wa masuala ya ujasiliamali lengo kuu ni kuwajengea uwezo Wanawake kujifunza elimu ya ujasiliamali ambayo ameona ndio ukombozi wa Mwanamke.
Alisema kutokana na upungufu wa ajira hususani kwa maeneo ya pembezoni hakuna budi elimu ya ujasiliamali ipate kuenezwa katika maeneo ya Vijijini ambayo itamfanya Mwanamke aweze kujitambua na kuelewa dhana nzima ya ujasiliamali ili uwe ni ukombozi kwa Mwanamke.
Nyagheti alisema Mwanamke ambaye atapata Elimu ya ujasiliamali anao uwezo mkubwa wa kupambana na majukumu ya kifamilia pasipo kuwa tegemezi na kuonekana mtu wa chini muda wote na kutegemea kila hitaji kumuomba Mwanaume nyumbani ama kumsubili mwanaume hata kama ametoka hata akiwa na hitaji la chumvi.
"Lizima Mwanamke aheshimike na hawezi kuheshimika kama ataendelea kuwa katika hali duni na kushindwa kujifanyia mahitaji yake hata madogo madogo,ntajitahidi kadri ya uwezo wangu kushirikiana na Wanawake wenzangu katika kujitafutia Maendeleo kwa njia ya kufanya ujasiliamali.
"Katika ziara yangu ya kutembelea Kata za Wilaya nzima ya Butiama nitakuwa na watu wa maendeleo ya Jamii pamoja na walimu wa masuala ya ujasiliamali nikiwa na lengo mahususi la kuwafikishie elimu Wanawake ili mwisho wa siku kila Mwanamke ambaye ajaajiliwa aweze kujiajili kupitia ujasiliamali,"alisema Nyagheti.
Mwenyekiti huyo wa UWT alisema Wanawake wa Wilaya ya Butiama na Kata ya Bwiregi wamempa heshima kubwa kumchagua kuwa Mwenyekiti wa Umoja wa Wanawake na wale walioshirikiana pamoja na Wanaume katika Kata ya Bwiregi kuwa Mwanamke pekee wa kuchaguliwa kama Diwani kati ya Kata 34 za Wilaya ya Butiama.
"Kwanza sina budi kusema Wanawake waliniunga mkono kwa asilia kubwa katika Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2010 nilipokuwa nagombea Udiwani katika Kata ya Bwiregi licha ya kuwa wapo Wanaume ambao pia waliniunga mkono katika kinyang'anyiro kile na Upinzania ulikuwa mkubwa sana.
"Kwa kuzingatia imani waliyoijenga kwangu nami sintowaangusha bali ntahakikisha najitahidi kila linalowezekana hasa kubwa ikiwa ni elimu ya ujasiliamali na kupeana njia za kuwezeshana kutoka kwa walimu na kujifunza sehemu mbalimbali ili mwisho wa siku kila mmoja awe na uchumi mzuri na kuweza kuendesha maisha ya kila siku,"alisema Mwenyekiti huyo. 
Alisema ziara amepanga kuanzia katika Tarafa ya Nyanja na kisha kumalizi katika Tarafa ya Kiagata na kudai kuwa licha kuambatana na walimu wa masuala ya ujasiliamali pia ataongozana na Viongozi wa Chama cha Mapinduzi Wilaya ya Butiama na kuwaomba Wananchi kufika katika mikutano yake kwani kutakuwa na faida kubwa watakayoipata.             " 

Post a Comment