1
 
MAHAKAMA ya Hakimu Mkazi  Mfawidhi  ya Wilaya ya Musoma mkoani Mara imetoa adhabu ya kuchapwa viboko 24  kwa watu wawili lucas Wancheka (17) na Saimoni Mnico(20) wakazi wa Bweri katika Manispaa ya Musoma waliokuwa wakituhumiwa kwa kosa la kubaka mwanafunzi wa shule moja ya sekondari mjini hapa.

Akisoma Hukumu hiyo mbele ya mahakama,Hakimu Mkazi Mfawidhi Ramadhani Rugemalira alisema kuwa watuhumiwa hao watachapwa viboko 12 kila mmoja baada ya Mahakama kuridhika na maelezo ya mashahidi saba wa upande wa mashitaka.

Rugemarira alisema shahidi wa kwanza ambaye ni mtendwa wa tukio hilo (Mwanafunzi) ambaye jina lake limehifadhiwa alidai mbele ya Mahakama kuwa Machi 23 mwaka 2012 majira ya saa 1:00 usiku akiwa anatoka shambani alikutana na vijana hao wawili aliowafahamu na kumshambulia kwa kumpeleka vichakani kisha kumfanyia unyama wa kumbaka kwa zamu.

Maelezo ya Shahidi huyo aliendelea kudai kuwa siku aliyofanyiwa unyama huo hakuweza kutembea kutoka katika kicha alichokuwa amevutiwa bali alijitaidi kutambaa hadi nyumbani kwa wazazi wake na kumuelezea mama yake mzazi yaliyomsibu.

Aliendelea kusema kuwa baada ya kumweleza mama yake kuhusiana na kitendo alichofanyiwa ndipo hapo mama mzazi alipochukuwa jukumu la kumpeleka mwanae kupata matibabu hosptali.

Kwa upande wake mwendesha mashitaka wa polisi Timoth Timoth aliiomba Mahakama kutoa adhabu kali kwa watu hao waliotenda kosa hilo kutokana na kukithiri kwa matukio ya ubakaji katika jamii.

Hata hivyo hakimu Rugemarila alihukumu kesi hiyo kwa kuzingaia kifungu cha sheria namba 131A (1 ),(2) na (3) kutokana na mtuhumiwa namba moja katika kesi hiyo kuwa na umri chini ya miaka 18.

Post a Comment

review buy tramadol next day - tramadol euphoria