0
 
     
    

Kivumbi cha mashindano ya Ester cup kwa mwaka wa tatu mfulululizo kimeanza kutimua vumbi katika uwanja wa sabasaba mjini hapa huku jumla timu 38 zikijitokeza kuwania kitita cha shilingi milioni moja.

Akifungua mashindano hayo ambayo kwa msimu huu yamekuwa na hamasa kubwa kutokana na kuongezwa kwa zawadi na timu zinazoshiriki,afisa michezo wa Wilaya ya Bunda Amosi Mtani alisema mashindano hayo yamekuwa na mafanikio makubwa tangu yalipoanzishwa mwaka 2011.

Alisema kupitia mashindano hayo kiwango cha soka katika Wilaya ya Bunda kimepanda na vipaji vingi vimeonekana kupitia michezo hiyo ikiwemo timu nyingi kujisajili kupitia ofisi ya michezo na utamaduni na hivyo kuongeza ushindani wa timu.

"Leo ni mwaka wa tatu mashindano haya yanafanyika na kila mmoja anaona mafanikio ambayo yameonekana kupitia mashindano haya ikiwemo wachezaji wengi walioipa ubingwa wa mkoa timu ya Polisi Bunda msimu huu wametokea katika mashindano haya.

"Kila mwaka bingwa wa soka mkoa wa Mara amekuwa akitoka Musoma lakini kwa msimu huu kwa zaidi ya miaka 15 tumeshuhudia bingwa akitoka katika Wilaya ya Bunda na bila kuuma maneno nikiwa kama afisa michezo wa Wilaya hii nampongeza sana Mbunge Bulaya kwa jitihada zake za kuibua vipaji na kuendeleza soka katika Wilaya hii,"alisema Mtani.

Afisa huyo aliwataka vijana kuyatumia mashindano hayo kuonyesha vipaji vyao nakucheza kwa malengo ya kufika mabli kutokea katika mashindano hayo ambayo yanafanyika kwa mwaka wa tatu mfululizo.

Katika michezo wa kwanza wa ufunguzi,timu ya Majengo fc iliisambaratisha timu ya Bunda yosso Academy kwa kuifunga mabao 4-2 kabla ya mchezo wa pili timu ya Guta fc kuibamiza timu ya panda miti mabao 3-0.

Bingwa mashindano hayo kwa mwaka huu ataondoka na kitita cha shilingi milioni moja pamoja na kombe,mshindi wa pili laki tano,mshindi wa tatu laki tatu,timu yenye nidhamu lakini moja huku mchezaji bora na mfungaji bora kila mmoja akichomoza na shilingi elfu hamsini.

Post a Comment