MWANAMKE mwenye ujauzito wa miezi sita mkazi wa Wilayani Tarime amepigwa
na anayedaiwa kuwa mume wake na kisha kufungwa katika zizi la ng'ombe
na kumsababishia majera pamoja na maumivu makali yaliyopelekea kukimbia
na kutafuta msaada katika vyombo vya kisheria na mashirika ya kutetea
Wanawake.
Tukio hilo limelipotiwa katika kituo cha msaada wa
kisheria kwa Wanawake na Watoto cha (CWCA) mjini Musoma baada ya mhanga
huyo kufika kwa ajili ya kuomba msaada wa kisheria kutokana na
manyanyaso ambayo amedai kufanyiwa na
mwanaume huyo kila wakati licha ya kuwa walishatengana.
Akizungumza
na BLOG HII ,Afisa Mwandamizi wa Shirika hilo Ostack Mrigo alisema
tukio la kupigwa kwa Mwanamke huyo lilitokea mwishoni mwa mwezi machi
mwaka huu na kumsabababishia mjamzito huyo ambaye jina
limehifadhiwa majeraha mwilini mwake kutokana na kufungwa katika zizi
pamoja na maumivu makali.
Mume anayedaiwa kumpiga mjamzito huyo
aliyefahamika kwa jina la Joseph Mwita (30) imedaiwa alishatengana na
Mwanamke huyo aliyezaa nae watoto watano kwa muda mrefu amekuwa na
mazoea ya kumpiga mara kwa mara kwa kumfata katika nyumba yake na
kumuunganisha vipigo hivyo pamoja na watoto aliyezaa nae.
Mrigo
ambaye ni mwanasheria wa Shirika hilo alisema siku ya tukio hilo mume
huyo alikwenda katika kikundi cha mwanamke huyo cha kusaidiana na
kuchangiana pesa na kuwataka wanakikundi wampe pesa za mwanamke na
kukataliwa na ndipo alipoenda nyumbani kwake nakuanza kumshushia kipigo
kisha kwenda kumfunga katika zizi la ng'ombe.
Alisema baada ya
kufikishiwa tukio hilo ofisini kwao waliamua kumpa msaada mwanamke huyo
kwa kufuatilia na kufanikiwa kumkamata mwanaume huyo na kumfungulia kesi
ya jinai katika mahakama mjini Musoma na sasa wapo kwenye
utaratibu wa kufungua kesi ya madai ya taraka pamoja mgawanyo wa mali
kwa kuwa alipomuacha mwanamke huyo hakutoa taraka.
Afisa huyo wa
(CWCA) alidai Shirika hilo litahakikisha linatoa msaada wa kisheria kwa
Mwanamke huyo kadri itakavyowezekana kwa kuwa mwanaume huyo amekuwa
akimnyanyasa mwanamke huyo kama alivyodai mwenyewe na kwa sasa ameamua
kutoka Tarime na kurudi kwao Kinesi Wilayani Rorya na bado hali yake
haijawa nzuri kutokana na kipigo alichopata.
Mrigo aliongeza kuwa
Shirika hilo kwa sasa linaendesha mafunzo ya Haki za Binadamu,Ukatili
wa Kijinsia,Sheria na vyombo vya utatuzi wa migogoro Nchini
yanayowashirikisha Wanawake na makundi mengine ili kuweza kuzijua haki
na kuelewa mahala pa kwenda pale panapotokea matatizo na migogoro ya
kisheria.
Alisema mafunzo hayo yanayofadhiliwa na Shirika la
Legal Service Facility yaliyoanza aprili 2 hadi 5 yatasaidia kwa makundi
mbalimbali katika jamii yanayokutana na vitendo vya ukatili
na unyanyasaji kuzijua haki zao na kupunguza vitendo vya ukatili
vinavyofanywa kwa Wanawake na Watoto ndani ya jamii.
Home
»
»Unlabelled
» MJAMZITO APIGWA NA KUFUNGWA KATIKA ZIZI LA NG'OMBE TARIME
Post a Comment
0 comments