DIWANI wa kata ya Buhare katika Manispaa ya Musoma kupitia Chama cha
Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) David Katikiro amemjia juu mkuu wa
Wilaya ya Musoma Jackson Msome kwa kitendo cha kuwakamata viongozi wa
kata yake pamoja na mjumbe wa Serikali ya mtaa na kumvurugia mkutano
ambao alikuwa ameuandaa.
Katika kauli yake mbele ya kikao cha
baraza la madiwani wa Manispaa ya Musoma,Katikiro alisikitishwa na
kukwazwa na kitendo cha Mkuu huyo wa Wilaya ambaye alihudhulia katika
mkutano wake aliokuwa ameundaa kuzungumza na Wananchi masuala
mbalimbali ya kata hiyo likiwemo suala la ulinzi shirikishi na
kuwakamata viongozi hao.
Alisema kutokana na kitendo
kilichofanywa na DC Msome kilipelekea mkutano wake kuvurugika na hivyo
kushindwa kuzungumza na Wananchi
ambao tayari walikuwa wamefika katika mkutano huo kujua kile ambacho
Diwani alitaka kuzungumza nao kwa kipindi hicho.
Diwani Katikiro
alidai alikwazwa na Mkuu huyo wa Wilaya kwa kitendo alichokifanya siku
hiyo kwani mara baada ya kuwakamata viongozi hao mkutano ulishindwa
kufanyika kwa kuwa kulikuwa na baadhi ya majibu ya maswali ya Wananchi
ambayo yalikuwa yanapaswa kutolewa na viongozi ambao aliwakamata na
kuondoka nao.
"Mheshimiwa DC pamoja na wajumbe wa baraza nipate
kusema sijawahi kukasirika na kukwazwa kama siku ambayo Mkuu wa Wilaya
alivuruga mkutano wangu ambao nilipanga kuzungumza na Wananchi ambao
wamenichagua ili niwatumikie.
"Hata kama sheria ilimpasa kufanya
hivyo kutokana na nafasi yake subira ilihitajika wakati ule maana kuna
masuala mbalimbali yalitakiwa kuzungumzwa katika mkutano ule ambao
ulivurugwa na Mkuu wa Wilaya,"alisema Diwani Katikiro.
Akijibu
hoja ya Diwani huyo,Mkuu wa Wilaya ya Musoma Jackson
Msome alisema ilimlazimu kuchukua maamuzi ya kuwakamata viongozi hao
baada ya kushindwa kusimamia majukumu yao yakiwemo masuala ya ulinzi
shirikishi katika kata ya Buhare.
Alisema katika kata hiyo
matukio ya mauaji kwa Wanawake yamekuwa yakijitokeza mara kwa mara huku
viongozi hao wakishindwa kusimamia majukumu yao pamoja na kuanzishwa kwa
ulinzi shirikishi utaratibu ambao umeanzishwa katika kila kata za
Manispaa ya Musoma.
"Diwani Katikiro hakunitendea haki kwa
kunishutumu na kudai nilimkuzwa kutokana na maamuzi niliyoyachukua
katika mkutano wake na Wananchi kwa sababu kata yake ndiyo inayoongoza
kutokea matukio ya mauaji na hata yeye kama Diwani hakuna hatua zozote
alizozichukua lazima tufanye kazi za Wananchi na tuache kulalamika
pasipo sababu,"alisema DC Msome.
Aidha madiwani katika kikao
hicho cha Baraza lililofanyika katika ukumbi wa mikutano wa Halimashauri
ya Manispaa ya Musoma walimtaka Mkuu wa Wilaya ya Musoma kuangalia
utaribu mzuri wa kuanzishwa kwa vikundi vya ulinzi shirikishi na kujua
iwapo mtu akipata tatizo akiwa katika ulinzi ni namna gani Serikali
itakavyo mshughulikia.
Home
»
»Unlabelled
» DIWANI CHADEMA MUSOMA AMJIA JUU DC MSOME
Post a Comment
0 comments