Serikali
inadaiwa kiasi hicho cha fedha zinazotokana huduma mbalimbali zilizotolewa na wazabuni
wa ndani kukupitia idara ya Magereza katika wizara ya mambo ya ndani ya
nchi,vyuo vya ualimu chini ya wizara ya elimu na mafunzo ya ufundi pamoja na
Tamisemi ikiwemo wizara ya afya kupitia vyuo vyake vyake vya Uganga mkoani
Mara.
Mwenyekiti
wa wazabuni mkoani Mara Edward Muhere,ameliambia gezeti hili kwa njia ya simu
kuwa deni hilo linadaiwa na wazabuni hao kuanzia mwaka 2009 hadi sasa na
Serikali imeshindwa kuonyesha nia ya dhati kulipa deni hilo.
Alisema kuwa
wazabuni wa mkoa wa Mara,wamekuwa wakitoa huduma mbalimbali katika taasisi hizo
vikiwemo vyakula katika magereza na vyuo hivyo bila ya kulipwa kwa kipindi
hicho,hatua ambayo sasa imewafanya wengi wao kufirisika kabisa na wengine kulazimika
kuuziwa nyumba zao na taasisi za fedha yakiwemo mabenki baada ya kushindwa kulipa
mikopo walikopa kwa biashara hiyo.
“Hivi hii
serikali sikivu kwa akina nani hasa,sisi wazabuni wa ndani ambao tumeonyesha
uzalendo wa hali ya juu wa kutoa huduma kwa mkopo kwa serikali yetu,lakini leo haitulipi
haki zetu kama wanavyolipwa wazabuni wa nje,tumevumilia vya kutosha sasa
tumechoka ngoja twende mahakamani”alisema Muhere na kuongeza.
“Watu
tumekopa mitaji benki tena kwa riba kubwa ili kufanya biashara hii,sasa tulio
wengi tumefirisika na wengine wamelazimika kuuziwa nyumba zao ili kulipa mikopo
ya benki lakini serikali imeshindwa kulipa fedha zetu huku sisi tukinyanyasika
kulipa kwa riba je hapa kuna haki kweli…nashauri watendaji wa serikali
wasifanye tuichukie serikali ya CCM ingawa tuna imani kubwa na Rais wetu Jakaya
Kikwete”alisema.
Mwenyekiti
huyo wa wazabuni mkoani Mara,alisema wakati wakiandaa taratibu za kuifikisha
serikali mahakamani wamekubaliana kusitisha kutoa zabuni kwa taasisi hizo ili
kuhakikisha serikali inawatendea haki wazabuni wa ndani kama inawatendea
wazabuni wengine wa nje ya nchi.
“Baadhi ya viongozi
wa wizara wao hawana matatizo kwani wanatambua deni hili tatizo kubwa lipo
hazina sasa sijui wanataka hadi sisi tutoe rushwa ndo tulipwe haki zetu za
msingi…kwa kweli serikali ijaribu kuwa na huruma na watu wake,hatuwezi kufisika
kiasi hiki na serikali ikaendelea kucheka kuwauawa watu wake hii ni hatari
kubwa na nchi inayojiita ya utawala bora na ambayo inadai kutenda haki”aliongeza
Muhere.
Mmoja ya wakuu
wa idara katika moja ya moja ya wizara hizo zinazodaiwa ambaye aliomba
kutotajwa gazetini,alipopigiwa simu kuthibitisha kama kweli idara yake ni
miongoni mwa wadai hao,alikiri kuwa deni hilo lipo lakini tatizo kubwa ni
hazina huku siasa pia ikitumika kuchelewesha ulipaji wa madeni hayo.
“Ndugu yangu
tunatambua tunadaiwa tena si kiasi hicho tu ni kikubwa zaidi kwa nchi nzima,lakini
baadhi yao wanalipwa sasa sijui kutokana na mahusiano na wakubwa huko juu,lakini
pia hazina ni tatizo kubwa kwa kweli,wanaweza kuifanya serikali katika siku za
usoni ikaja kulipa deni kubwa zaidi kama watu hawa wakianza kudai deni lao kwa
riba”alisema kiongozi huyo.
Mwishoni mwa
mwaka jana katibu mkuu wa wizara ya elimu na mafunzo ya ufundi Selestine
Gesimba,alipoulizwa kuhusu deni hilo alikiri kuwa wizara yake inadaiwa na
kwamba taratibu zinafanyika kwaajili ya kuhakikisha deni hilo linalipwa lakini
hadi sasa hakuna kilicholipwa.
Post a Comment
0 comments