0










  Bw Joseph Mtalemwa -Menaja wa Tigo kanda ya Ziwa alipokuwa akitoa salamu katika maazimisho ya uchangiaji damu ambapo kitaifa yalifanyika mkoani Mara.




Bw Joseph Mtalemwa -Menaja wa Tigo kanda ya Ziwa
Kampuni ya simu za mkononi ya Tigo imepongezwa na Wananchi kwa kuwa mstari wa mbele kushiriki katika huduma za kijamii ikiwemo ya hivi karibuni ya kampeni ya kuchangia damu ambayo kitaifa ilifanyika mkoani Mara na kuhudhuliwa kwa wingi na watu mbalimbali akiwemo Naibu Waziri wa Afya na Ustawi wa Jamii Balozi Seif Suleiman Rashid.

Wakizungumza kwa nyakati tofauti na blog hii,walidai katika makampuni ya simu hapa Nchini Tigo imekuwa ikishiriki katika shughuli mbalimbali za kijamii na kutoa mchango katika kulijenga Taifa.

Kutokana hamasa ambayo tigo ilishiriki katika uchangiaji wa damu ilipoelekea mkoa wa Mara kuvuka lengo la makusanyo ya damu katika mkoa ambapo naibu Waziri wa Afya alipozungumza na blog hii baada ya kilele cha maazimisho ya uchangiaji damu alitaka makampuni mengine kuiga mfano wa kampuni ya Tigo katika kushiriki katika shughuli za kijamii.

                                              soma makala ya damu
 
KILA tarehe 14 juni Dunia inaazimisha siku ya wachangia damu duniani(World Blood Donor Day) ikiwa na lengo la kuwashukuru na kuwatambua wale wote ambao kwa kuelewa umuhimu wa damu salama huwa wanajitolea kuchangia damu kwa hiari.

Jamii inahimizwa kuchangia damu ili kuokoa vifo hususani vya mama wajawazito na watoto wachanga vinavyotokea wakati wa kujifungua huku tatizo kubwa la vifo hivyo ikitajwa kuwa ni damu.

Takwimu zinaonyesha kina mama 48,000 na watoto 8,000 ufariki dunia kutokana na upungufu wa damu hapa Tanzania,kiwango ambacho ni kikubwa kuliko nchi yoyote duniani kwa mujibu wa wataalamu wa afya.

Kiasi cha chupa 450,000 za damu zinahitajika kwa mwaka Nchini Tanzania huku kiasi kikubwa kikitumika kuokoa maisha ya mama na watoto lakini cha kusikitisha chupa 150,000 za damu ndizo zinazopatikana na kusambazwa.

Kwa mujibu wa takwimu za Shirika la Afya Duniani (WHO) zinaonyesha jumla ya damu zinazotolewa kila mwaka ulimwenguni kwa utaratibu wa kujitolea ni chupa milioni 80.

Katika idadi hiyo niliyoitaja nchi zinazoendelea ikiwemo Tanzania hutoa asilimia 38 tu idadi ambayo haiendani na asilimia 82 ya wagonjwa ambao tiba yao ina uhitaji wa damu.

Imebainishwa wagonjwa wenye uhitaji wa damu kwa wingi ni watoto chini ya miaka mitano,wanawake wajawazito,watu wanaopata ajali pamoja na wale wenye magonjwa mbalimbali yanayosababisha upungufu wa damu.

Tunaweza kuokoa vifo vinavyotokana na upungufu wa damu kwa kujitoa kuchangia damu kwani kitendo cha kuchangia damu ni kitendo cha kibinadamu kwani kinaokoa maisha ya binadamu.

Damu salama maana yake ni ile damu ambayo haina vimelea vya maradhi ambayo yanaweza kuambukiza mtu mwingine iwapo mtu huyo ataongezewa.

Maradhi ambayo yametajwa na kuweza kuambukiza kupitia kwenye damu ni Ukimwi (HIV),Homa ya Ini (Hepatitis) pamoja na Kaswende (Syphilis) ambayo yanachunguzwa na vituo vya damu salama vilivyopo kila kanda.

Majukumu makuu ya vituo vya damu salama vinatakiwa kuhakikisha malengo ya upatikanaji wa damu salama yanafikiwa ikiwa ni pamoja na kutoa uhamasishaji kwa jamii ili kuweza kuchangia.

Lakini licha ya kuhamasisha jamii kujitoa kuchangia damu kitu muhimu kinachopaswa kufanywa na vituo vya damu salama ni kuhakikisha damu inapimwa kwa usahihi na kwa utaalamu wa hali ya juu ili kuhakikisha usalama wake.

Nikirejea katika suala la kuchangia watu wengi hawatambui umuhimu wa kujitolea kuchangia damu katika kuokoa maisha ya binadamu ili hatimaye kila mtu mwenye afya nzuri awe mchangiaji damu wa mara kwa mara.

Katika uzinduzi wa kampeni ya kuchangia damu mkoani Mara iliyofanyika Wilayani Bunda,mkurugenzi wa Shirika la (Evidence For Action) Craig Ferla linaloshughulika na kampeni ya uchangiaji wa damu Tanzania alisema vifo vya akina mama na watoto wachanga wakati wa kujifungua ni vingi hapa Nchini kuliko sehemu nyingine Duniani hivyo wanaweza kuokolewa kwa kuchangia damu.




  




Post a Comment