0



















KADA wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) wilayani Bunda maarufu kama Kamanda Pius amesema lengo lake ni kuhakikisha vipaji vya vijana katika Wilaya hiyo vinainuka na kuwa ni moja ya njia za kuongeza ajira kupitia michezo.

Pius alitoa kauli hiyo mwishoni mwa wiki iliyopita alipokuwa akikabidhi zawadi mbalimbali za vikombe mipira,jezi pamoja na fedha taslim kwa mashindi wa mashindano ya Pius Cup yaliyomalizika wilayani Bunda katika uwanja wa sabasaba.

Amesema ataendelea kuboresha mashindano na kuongeza zawadi katika mashindano hayo ambayo amepanga kuyafanya kila mwaka ili kuongeza chachu ya  na kuwafanya vijana wengi kujitokeza kushiriki.

Katika fainali ya mashindano hayo timu ya Amani fc iliibuka mabingwa kwa kuifunga Kiwasi fc kwa changamoto ya penati 5-4 baada ya kumalika dakika 120 bila timu hizo kufungana.

Kwa kuibuka mabingwa,timu ya amani ilikabidhiwa kikombe kikubwa,medali pamoja na fedha taslimu shilingi laki sita huku washindi wa pili wakichomoza na laki nne pamoja na kikombe.

Zawadi nyngine zilikwenda kwa mshindi wa nne shilingi elfu hamsini,mshindi wa tatu laki mbili,timu bora ilichukua kikombe pamoja na mpira,mchezaji bora,kipa bora,mfungaji bora pamoja na timu yenye nidhamu kila mmoja alipata kikombe,medali pamoja fedha taslim shilingi elfu ishirini

Post a Comment