0
 
 
WAZAZI na Walezi wametakiwa kuzingatia malezi bora kwa vijana ili wasije kujiingiza katika matumizi ya dawa za kulenya kwa kuiga tabia za makundi hatarishi na kupoteza nguvu kazi ya Taifa. 

Kauli hiyo ilitolewa na Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi Wilaya ya Rorya Samwer Kiboye katika mahafari ya tano ya dalasa la saba ya shule ya msingi Emanuel iliyopo Manispaa ya Musoma.

Alisema kutokana na wimbi la kuzuka kwa kasi kwa matumizi ya dawa za kulevya ni wajibu wazazi na walezi pindi wanafunzi wanapohitimu elimu ya msingi na kuwa nyumbani kuwalea katika malezi bora ili wasijiingize katika makundi hatarishi.

Kiboye alisema katika kipindi hicho ni vyema wanafunzi kuwapa masomo ya ziada kuliko kuwa mitaani hali ambayo inaweza kuwafanya kuingia kwenye makundi ya vijana  ambao bado hawajabadilika na kushiriki vitendo vibaya.

Alisema kwa sasa Taifa limekuwa kwenye mjadala na mapambano dhidi ya madawa ya kulevya na athari ya matumizi yake hivyo kila mmoja anapaswa kuchukua hatua kupingana nayo.
Alisisitiza kuwa madawa ya kulevya sio cocaine na mengineyo bali hata bangi ni dawa za kulevya na ndio vijana wengi wamejiingiza katika matumizi yake na kuharibikiwa.

Aidha Mwenyekiti huyo CCM Wilaya ya Rorya aliyekuwa mgeni rasmi kwenye mahafari hayo ya shule ya msingi Emanuel aliwataka wanafunzi wanaohitimu elimu ya msingi katika shule hiyo kuwa watulivu katika chumba cha mtihani ili waweze kufanya vizuri na hatimaye kujiunga na elimu ya sekondari hapo mwakani.

Kwa upande wake Mkurugenzi wa shule hiyo Ester Marwa alisema hazina kubwa ambayo anastahili mtoto kwa sasa ni elimu hivyo kuwaomba wazazi kuhakikisha vijana wanakuwa na elimu bora kuanzia msingi,sekondari hadi vyuoni.
 
 

Post a Comment