0
AFISA MASOKO MWANDAMIZI WA POSTA MAKAO MAKUU KALOLINE KANUTI AKIWA NA WATOTO WA KITUO CHA MTAKATIFU JUSTINE BAADA YA KUTOA MSAADA



 MENEJA WA PSTA AKIWA KATIKA PICHA YA PAMOJA NA VIJANA WA KITUO CHA MTAKATIFU JUSTINE NA WAFANYAKAZI WA POSTA

MENEJA WA SHIRIKA LA POSTA MKOA WA MARA BAKARI KOMBO BAKARI AKIMKABIDHI MISAADA MBALIMBALI YA KIJAMII MLEZI WA KITUO CHA KULEA WATOTO WENYE ULEMAVU WA AKILI NA VIUNGO CHA MTAKATIFU JUSTINE SISTER MAGRETH JOHN

MWENDO WA MCHELE MBUZI
WATOTO WENYE UHITAJI TUWAKUMBUKE
LECHA YA ULEMAVU WATOTO HAWA WASIO SIKIA WALISHIRIKIA MASHINDANO YA KITAIFA YA RIADHA JIJINI DAR ES SALAAM
PAMOJA TUWALEE


LICHA ULEMAVU ANAFANYA VIZURI SANA DARASANI
Jamii imetakiwa kujenga utamaduni wa kusaidia watu walio kwenye uhitaji ili waweze kuondokana na matatizo mbalimbali yanayowakabili na kuifanya jamii husika kuishi kama binadamu wengine bila kujiona wanyonge na wapweke waliosahalika.

Kauli hiyo imetolewa na Meneja wa Shirika la Posta mkoani Mara Bakari Kombo Bakari alipokuwa akikabidhi misaada mbalimbali ya kijamii ikiwemo mchele,mbuzi mnyama,mafuta ya kupikia pamoja na sabuni katika kituo cha kulea watoto wenye ulemavu na yatima cha Mtakatifu Justine kilichopo Manispaa ya Musoma ikiwa ni maadhimisho ya siku ya posta duniani.

Amesema kwa namna walivyokitembelea kituo hicho na kukutana na changamoto mbalimbali zinazowakabili  jamii inapaswa kuona umuhimu wa kuwasaidia ili waweze kuondokana na adha zinazowakabili katika kituo hicho.

Meneja huyo wa posta amesema watoto wenye ulemavu ukiwemo wa akili,viziwi na viungo walipo kwenye kituo hicho wanahitaji misaada ikiwemo chakula na mahitaji mengine kwa mujibu wa wasimamizi wa kituo hicho hivyo jamii inapaswa kuliangalia na kuona umuhimu wa kuwasaidia.

Amesema Shirika la posta ikiwa ni moja ya jukumu lao kutoa misaada katika jamii yenye uhitaji lakini kazi hiyo haiwezi kufanya na upande mmoja bali kila mmoja anawajibika kuguswa na changamoto walizonazo watoto hao na kuweza kuwasaidia

Kwa upande wake Muangalizi mkuu wa kituo hicho sister Magreth John amelishukuru Shirika la posta kwa msaada waliopa baada ya kuwatembelea na kuomba watu wengine kuguswa na mazingira waliyokuwa nayo watoto wenye ulemavu na yatima na kuwapa msaada wa kibinadamu.

Amesema kituo hicho chenye jumla ya watoto 130 wenye ulemavu mbalimbali wanakabiliwa na uhaba wa chakula kwenye kituo nakusema mtu yoyote anaweza kuwatembelea kwenye kituo hicho kilichop[o makoko na kuwapa msaada.

Post a Comment