Askofu wa Kanisa la Anglikana Jimbo
la Rorya John Adiema,amefunguliwa mashitaka na mke wake ambapo pamoja na mambo
mengine Mwanamke huyo ameiomba Mahakama ya Hakimu Mkazi mkoa wa Mara kutengua
ndoa yao na kupewa talaka.
Kesi hiyo ambayo ni ya kwanza kutokea Nchini kwa Kanisa hilo
kuhusu Askofu kufikishwa Mahakamani imepangwa kusikilizwa novemba kumi na nane
mwaka huu katika Mahakama hiyo mjini Musoma.
Mke
huyo wa Kiongozi Mkuu wa kanisa la Angilikana Jimbo la Rorya Peres
Adiema,akizungumza baada ya kufungua shauri hilo Mahakamani hapo,alisema
pamoja na talaka pia anamdai mume wake huyo haki zake za msingi
walizochuma
wakiwa kama wana ndoa.
Mama huyo alidai amefikia
uamuzi wa kudai talaka baada ya kuishi katika manyanyaso kwa muda wa miaka 12
sasa bila kujua hatima ya manyanyaso hayo ni lini,hivyo amefungua kesi ya madai
namba moja katika mahakama ya mkoa na kupangwa kuanza kusikilizwa novemba
18 mwaka huu.
Alisema chanzo cha yeye kudai
talaka yake Mahakamani ni hatua iliyochukuliwa na mume wake ambae ni Askofu ya
kumtaka aache kazi ili waweze kuendelea kuishi pamoja ili hali awali kabla
hajaolewa na baada ya kuolewa alikuwa ni muuguzi katika hosptali ya Misheni ya
Kowaki Rorya inayomilikiwa na kanisa la Romani Katoliki.
Alidai baada ya kufunga ndoa na
Askofu huyo ambaye hapo awali alikuwa Mchungaji katika Kanisa la Anglikana Musoma
alitafuta uhamisho wa kutoka Rorya ili aweze kufanya kazi akiwa karibu na
mumewe,ambapo hakufanikiwa kupata tena kazi ya Uuguzi.
Peres alisema baada ya kuishi na
mumwe kwa muda wa mwaka mmoja wa ndoa mume huyo alianza kumtaka aache
kazi ili waweze kuendelea kuishi pamoja la sivyo atoke kwake,jambo ambalo
alidai lilimsumbua sana akili,hivyo akaamua kuacha kazi na kukaa nyumbani.
Alida baada ya kukaa nyumbani
mume huyo alikuwa akimfanyia manyanyaso ambayo hakutarajia kuyapata kutoka kwa
mtu mwenye hadhi aliyokuwa nayo mumewe kama mchungaji,hivyo alichukua uamuzi wa
kutafuta tena ajira upya ili aweze kuondokana na manyanyaso madogo madogo.
Alisema alifanikiwa kupata ajira
katika Hospitali ya Mkoa ambapo hata hivyo mumewe aliendelea kumsumbua hadi kwa
mwajiri wake kwa kuweka shinikizo la kumwachisha kazi hali amabayo alidai ilikuwa ikimpa wakati mgumu katika utendaji kazi.
“Ilifikia hatua akanifukuza
kwake,akaniambia nichague….kama nataka kazi niishi na kazi kama nataka
ndoa niache kazi ili niiweze kuishi nae,nami nikaona ni msalaba ni bora
nikaishi mwenyewe maisha yangu”alidai mama huyo huku akibubujikwa na machozi.
Peres alidai mwaka 2012
alichukua uamuzi wa kuondoka,ambapo Askofu huyo alikatalia watoto wawili aliozaa naye,mkubwa akiwa na umri wa miaka tisa na mdogo akiwa na miaka saba
huku akimyima ruhusa ya kuonana na watoto hao.
“Nilizaa na Askofu watoto wawili
ambao niliwaacha,lakini hata hao watoto nikisia ni wanaumwa kiasi gani sina
ruhusa ya kuwaona na hata hataki kuniona nikiwa nyumbani kwake ndio maana nimeomba talaka na
mahakama itoe uamuzi ambao itaona unafaa”alisema Peres.
Kiongozi mmoja wa dini wa kanisa
hilo ambaye aliomba kutotajwa
gazetini,alisema sheria za kanisa hilo zinasema endapo kiongozi wa juu (Askofu)
akifikishwa Mahakamani kwa kosa kama hilo anapaswa kujihudhulu nafasi hiyo au
kufukuzwa ndani ya kanisa.
“Sheria ziko wazi, sasa kama askofu
anafikishwa Mahakamani kwa kosa la unyanyasaji na kushindwa kuimudu familia
yake sasa itakuwaje kwa kondoo anaowaongoza…hivyo kufikishwa mahakamini tu kwa
madai kama hayo kunamuondolea hadhi yake ya kuwa kiongozi wa kanisa”alisema.
Post a Comment
0 comments