0



JUMLA ya wapatao 946 chini ya miaka mitano  mkoani Mara wamepoteza maisha kutokana  na ugonjwa wa malaria katika kipindi cha Januari hadi Desemba mwaka 2012.
 
Mkuu wa Wilaya ya Musoma Jackson Msome kwa niaba ya mkuu wa mkoa wa Mara John Tuppa aliyasema hayo wakati akifungua kikao cha uhamasishaji wa kampeni ya kunyunyizia  dawa ya kuua mbu waenezao malaria majumbani awamu ya pili mzunguko wa tatu kilichofanyika kwenye ukumbi wa uwekezaji mkoani Mara.
 
Tuppa alisema kuwa malaria bado ni ugonjwa hatari unaoenendelea kupoteza maisha ya watu wengi na kwamba wastani wa mtu mmoja anapoteza maisha kwa kila dakika ambapo kitaifa wastani wa wagonjwa 60,000 hupoteza maisha kwa mwaka kutokana na ugonjwa huo.
 
“Hatuna budi kupambana na Ugonjwa huu ambao ni hatari hasa zaidi kwa watoto wenye umri chini ya miaka mitano ,akina mama wajauzito,wazee na wagonjwa wenye magonjwa sugu kutokana na kinga za mwili kuwa chini”,Alisema Mkuu huyo wa mkoa.
 
Kuhusu  takwimu alisema kuwa zinaonyesha kuwa katika mkoa wa Mara uambukizi wa malaria kwa watoto upo katika asilimia 25 ukilinganishwa na mikoa jirani ya kanda ya ziwa kama vile Mwanza ,Geita, Kagera na Simiyu
 
Kutokana na ukubwa wa tatizo hilo hasa kwa kanda ya ziwa serikali kupitia kitengo chakupambana na malaria  chini Wizara ya afya na ustawi   wa jamii kupitia mfuko wa rais wa Marekani chini ya shirika la misaada la watu wa Marekani (USAID)inatekeleza mradi wa upulizaji dawa ya kuua mbu majumbani.
 
Mratibu wa Malaria mkoa wa Mara, Tukae Lisso alisema kuwa  lengo ni kukumbushana na kuwahamasisha juu ya mabadiliko katika zoezi la IRS kwa mwaka 2013 mzunguko wa pili  na kutoa malengo ya zoezi hilo kwa mkoa wa  Mara katika wilaya zilizokusudiwa .
 
Aliongeza kuwa   kutakuwa na wahamasishaji wa  jamii ili waweze kushiriki kikmilifu na kuweza kujiandaa   katika zoezi hilo ili kupunguza kiwango cha malaria kwa kutumia wahusika katika eneo lililopo katibu na mazingira yao.
 
Katika awamu ya mzunguko wa tatu awamu ya  pili lengo ni kupulizia kaya 24698 katika wilaya za Rorya,Tarime na Serengeti mkoani humo ambapo mradi huu kwa mwaka huu umeweka makazi yake katika wilaya ya Rorya kama sehemu ya majaribio.

Post a Comment