0

TAASISI ya Kuzui na Kupambana na Rushwa mkoani Mara (TAKUKURU) inamshikilia Mkurugenzi wa kituo cha Makoye Education Centre kilichopo maeneo ya Nyasho Manispaa ya Musoma Mwalimu Joseph Makoye  kwa tuhuma za kudai Rushwa ya ngono.

Inadaiwa Mkurugenzi wa kituo hicho alidai Rushwa ya ngono kwa mwanafunzi aliyekuwa akifanya maandalizi yake mtihihani wa Taifa wa kidato cha nne 2013 katika kituo hicho mtihani unaoanza leo.

Katika taarifa iliyotolewa kwa vyombo vya habari na mkuu wa Takukuru mkoa wa Mara Holle Makungu ilidai mwanafunzi huyo wa kie ambaye jina lake linahifadhiwa alijiandikisha kufanya mtihani huo kupitia sanduku la posta 216 la kituo hicho ambapo barua yake ya mtihani kutoka Baraza la Mtihani ilipitia katika kituo hicho na ndipo Mkurugenzi wa kituo hicho alipotaka apewe rushwa ya ngono ili aitoe barua hiyo.

Taarifa hiyo ilidai baada ya barua hiyo kupokelewa katika kituo hicho ilishikiliwa na mtuhumiwa ambaye kimsingi  ndiye mmiliki  wa sanduku hilo la barua kwa jina la Makoye Education Centre na kushindwa kumpa binti huyo hadi apewe Rushwa ya ngono ikiwa ni sharti la kuipata barua hiyo.

Iidai taarifa hiyo kuwa mtuhumiwa alitoa tahadhari ya kama binti huyo hatatoa Rushwa hataweza kufanya mtihani wake kwa kuwa asingempatia barua hiyo toka Baraza la Mitihani la Tanzania.

Kututokana na hali hiyo ya kuombwa Rushwa ya ngono binti huyo alikwenda kutoa taarifa Takukuru ambapo iliandaa mtego wa kumnasa mtuhumiwa huyo kati eneo kilichopo kituo hicho octoba 2 majira ya saa 1 usiku baada ya mtuhumiwa kumpigia simu mwanafunzi huyo na kumtaka aende hapo.

Mkuu wa Takukuru Mara alidai maafisa wa Taasisi hiyo wakiwa katika mtego wao alifika mtuhumiwa katika eneo hilo kisha kumuita mwanafunzi na kumpandisha kwenye gari namba T 697 BNQ kisha kwenda naye katika nyumba ya kulala wageni ya Tedasi iliyopo eneo la Bweri nje kidogo ya mjini wa Musoma huku wakiwa na tahadhari ili mwanafunzi huyo asiweze kufanyiwa mabaya.

Taarifa hiyo ya Takukuru iliendelea kueleza kuwa Makachero wa Takukuru walifanikiwa kumtia mbaroni mtuhumiwa huyo katika nyumba hiyo ya wageni kisha kwenda nae nyumbani kwake eneo la Mkendo Kati na kufanya upekezi na kufanikiwa kuipata fomu hiyo kutoka Baraza la Mtihani la Taifa.

Holle alidai uchunguzi zaidi wa tukio hilo bado unaendelea na mara utakapokamilika hatua zaidi za kisheria zitachukuliwa dhidi ya mtuhumiwa huku akitoa wito kwa mabinti na wanafunzi wanaokutana na visa vya unyanyasaji wa kijinsia kuwa na uthubutu wa kutoa taarifa ili wanaohusika waweze kuchukuliwa hatua za kisheria

Post a Comment