WANANCHI wanaoishi kandokando ya Hifadhi ya Serengeti mkoani Mara, wanahitaji msaada wa haraka wa chakula
kutokana na uvamizi wa mashamba na maghala ya kuhifadhia chakula uliofanywa na
tembo kutoka hifadhi hiyo walio wavamia.
Katibu wa Kamati ya madiwani wa Chama cha Mapinduzi wilayani Serengeti Richard Nyakera, alikiambia kikao
cha Baraza la madiwani wa Halmashauri ya Wilaya hiyo kuwa Wananchi
waishio katika kata nane za Halmashauri hiyo wanakabiliwa na njaa.
Nyakera
alizitaja Kata ambazo
uvamizi huo wa makundi ya tembo umesababisha upungufu wa chakula ni Kata
za Sedeco, Manchira, Kyamba, Nyansurura, Machochwe, Natta, Isenye na
Ikoma na kudai kama jitihada za haraka hazitafanywa na Serikali huenda
vikatokea vifo vya Wananchi kutokana na njaa.
Alisema pamoja na kuomba msaada huo
wa chakula kamati hiyo ilisema kwa vile Serikali inafanya doria kupambana na
majangili basi pia ifanye kila juhudi kuhakikisha kuwa tembo hao
wanarudishwa hifadhini na kuwatoa katika maeneo ya Wananchi ambao wanatishia maisha yao pamoja na kuharibu chakula.
Katibu huyo wa madiwani wa CCM ambaye pia ni Diwani wa Kata ya Sedeco alisema Serikali
wilayani humo inatakiwa kutangaza tatizo la upungufu wa chakula wilayani
humo sasa ni janga hivyo kuhitaji hatua za haraka kuokoa maisha ya
wananchi.
Kwa
upande wake Diwani wa Kata ya Manchira Michael Shaweshi (CCM) alisema
suala la uvamizi wa tembo katika makazi ya Wananchi na kuharibu mashamba
pamoja na chakula ambacho tayari kimehifadhiwa kwenye maghala sio la
kulikalia kimya na Serikali kupitia Wizara ya Mali Asili na Utalii
wanapaswa kuchukua hatua za makusudi kukabiliana na hali hiyo.
Alisema
makundi ya tembo kwa sasa yamekuwa yakiingia hadi katika maeneo ambayo
awali walikuwa hawafiki jambo ambalo linatishia zaidi mazao ya wakulima
pamoja na maisha yao na kudai kwa sasa tayari tembo hao wameshaharibu
mashamba mengi ya Wananchi na kuwaacha wakikabiliwa na njaa.
Shaweshi
alisema kutokana na hali hiyo kuna kila sababu kwa Halimashauri ya
Wilaya ya Serengeti kutangaza baa la njaa kutokana na uhalibifu mkubwa
ambao umefanywa na tembo ambao walitoka hifadhini na kuvamiwa mashamba
ya Wananchi na kuharibu mazao.
Katika
kikao hicho cha Baraza la madiwani kilichofanyika kwenye ukumbi wa
mikutano wa Halimashauri hiyo ya Serengeti kiliandaa Sheria ndogondogo
zilizotungwa chini ya kifungu cha 168 juu ya taratibu za Ufugaji,Ulinzi
na Usalama,Afya ya Jamii,Elimu,Ushiriki katika shughuli za Maendeleo na
kilimo za Halimashauri ya Kijiji ili kuondokana na matatizo mbalimbali
ya wagugaji na Hifadhi ya Serengeti pamoja na masuala ya Wananchi.
Post a Comment
0 comments