0

 MAMBO YALIANZA NA KIKAO CHA WAJUMBE WA HALIMASHAURI KUU YA WILAYA
 KADA WA CCM MZEE NYAKEKE
 MBUNGE WA JIMBO LA RORYA LAMECK AIRO AKIZUNGUMZA

 KULIA NI MWENYEKITI WA CCM MKOA WA GEITA JOSEPH MSUKUMA

 KISHA UKAPIGWA MSOSI

 BAADAE UELEKEO ULIKUWA UWANJA WA NYANDUGA KUSHUHUDIA FAINALI ZA LA KAIRO CUP 2014 ZILIZOENDANA NA MAAZIMISHO HAYO

 TIMU YA UTEGI FF NA NYANDUGA FC ZIKIINGIA KWA AJILI YA MSCHEZO WA FAINALI AMBAPO TIMU YA UTEGI WALIIBUKA MABINGWA NA KUJINYAKULIA MILIONI TANO
 UKAGUZI

 MSUKUMA AKISALIMIANA NA MCHEZAJI WA UTEGI FC
 SALAMU ZA FAIL PRAY NI MUHIMU KABLA MCHEZO KUANZA
 MBUNGE AIRO GOLINI
 MSUKUMA AKIENDA KUPIGA PENATI
 HAPA BAO LILIFUNGWA

 HAPA PENATI YA MWENYEKITI WA CCM RORYA NAMBA TATU ILIDAKWA

 KIPA KUSHOTO MPIRA KULIA
 FURAHA YA UBINGWA
 AIRO AKIZUNGUMZA BAADA YA FAINALI


CHAMA cha Mapinduzi (CCM) kimesema hakitasita kuwasema na kuwafikisha kwenya vikao vya maadili watumishi ambao watashindwa kufanya kazi zao na kutekeleza ilani ya uchaguzi ya chama hicho na kupelekea kulalamikiwa na Wananchi.

Akizungumza katika mkutano wa maazimisho ya miaka 37 ya CCM wilayani Rorya,Mwenyekiti wa Chama cha  Mapinduzi mkoa wa Geita  Joseph Kasheku ‘Msukuma’alisema wataizingatia kauli ya Rais Jakaya Kiwete aliyoitoa mkoani mbeya kutomuonea aibu mtumishi na kufatilia kwa karibu utekelezaji wa ilani.

Alisema kamwe hawatakubali kuona watumishi wazembe na wanaojiingiza kwenye siasa kukwamisha shughuli za maendeleo kwa kutosimamia miradi huku shutuma zikielekezwa kwa Serikali ya CCM.

Msukuma alisema katika siku za hivi karibuni kumeibuka taarifa za kuhusu Chama cha Mapinduzi(CCM) wilayani Rorya kulalamikia utendaji kazi wa Mkuu wa Wilaya hiyo pamoja na Mkurugenzi na kusema ili kazi ziweze kwenda ni lazima viongozi wa CCM wawe wakali katika kusimamia ilani.

Mwenyekiti huyo wa CCM mkoa wa Geita ambaye alikuwa mgeni rasmi katika maazimisho hayo yaliyofanyika kiwilaya katika uwanja wa Nyanduga,aliwataka viongozi wa CCM Wilaya ya Rorya kutokusita kuzungumza kila wanapoona uzembe wa watumishi.

"Niwashukuru sana viongozi wa Chama Wilaya kwa kusimamia utekelezaji wa ilani na kutokusita kuwazungumza viongozi ambao wanakwamisha shughuli za maendeleo na kupelekea chama kulaumiwa.

"Mwenyekiti wa Wilaya Samwer Kiboye"namba tatu,Mbunge Lameck pamoja na viongozi wengine wa hapa Rorya muendelee na msimamo huo wa ufatiliaji wa utekelezaji wa ilani na sisi tuko nyuma yenu hakuna haja ya kumuogopa mtumishi yoyote asiyetekeleza majukumu yake",alisema Msukuma.

Kwa upande wake Mwenyekiti wa CCM Wilaya ya Rorya Samwer Kiboye alisema wapo watumishi ambao wamejiingiza katika siasa na kushindwa kufanya kazi kutokana na taaluma yao ambao ndio kikwazo cha kufanya chama hicho kulaumiwa.

Alisema wapo watendaji ambao wanaanza kujadili Rais ajaye wakiwa ofisini na kushindwa kutekeleza majukumu yao na kudai Rais ni mmoja Jakaya Kikwete na hawata muonea haya mtumishi yoyote asiyewajibika.

Mwenyekiti huyo alipongeza hotuba ya Rais kikwete aliyoitoa mkoani Mbeya katika maazimisho ya miaka 37 ya CCM iliyowataka viongozi wa chama hicho kuhakikisha wanafatilia kwa karibu utekelezaji wa ilani.

Kwa upande wa masuala ya michezo,Mbunge wa Jimbo la Rorya Lameck Airo alisema kila mwaka ataendelea kubolesha musuala ya michezo hususani kombe la Lamec ambapo kwa mwaka huu amedai kutumia zaidi ya milioni 30 ili kufanikisha mashindano hayo.

Alisema michezo licha ya kuwa nia ajira na kukuza vipaji pia anaitumia kama sehemu ya kuwaweka vijana pamoja na kushindwa kwenda kujiunga na makundi ambayo hayai katika jamii

Post a Comment