0

USALAMA KWANZA

Maeneo ya uwezaji mkoa wa Mara


WANANCHI mkoani Mara wametakiwa kushirikiana na jeshi la polisi kuhakikisha mkoa pamoja na wilaya zake unakuwepo usalama wa kutosha ili kuweza kuwavutia wawekezaji kuja kuwekeza kutokana na fursa nyingi za uwekezaji zilizopo.

Kauli hiyo ilitolewa na mkuu wa kitengo cha Polisi Jamii mkoa wa Mara kamishina msaidizi Claud Kanyorota alipokuwa akizungumza na Shommi Blog namna ambavyo kitengo hicho kilivyoweka mikakati kuhakikisha jamii inashirikiana na polisi kuweza kufichua wahalifu na uhalifu ili kuweza kuuweka mkoa katika hali ya usalama.

Alisema kamwe mwekezaji yoyote hawezi kukubali kwenda kuwekeza mahali ambapo usalama wake ni mdogo ambao unaweza kuvuruga uwekezaji wake na kuwataka wananchi wote wapenda maendeleo kuhakikisha wanalichulia suala la usalama kama mojawopo ya kivutio cha wawekezaji.

Kanyorota alisema mikakati iliyopo kwa sasa ya jeshi la polisi kupitia kitengo cha polisi jamii ni kuwa karibu na wananchi na kufundishana mbinu mbalimbali za kufichua wahalifu katika jamii ili matukio ya kiuhalifu yaweze kuondokana na kupata fursa ya kuweza kutoa nafasi watu mbalimbali kuja kuwekeza mkoa wa Mara.

Alisema mkoa wa Mara unazo fursa nyingi za uwekezaji katika sekta za madini,kilimo na hata maeneo ya ujenzi wa viwanda lakini watu wengi wamekuwa wakishitushwa na matukio ya kiuhalifu ambayo yamekuwa yakiwatisha wawekezaji kuja kuwekeza.

Ameongeza kuwa,fursa mbalimbali za uwekezaji mkoani Mara zilizotangazwa hivi karibuni kwenye mkutano wa kujadili fursa za uwekezaji kanda ya ziwa uliofanyika hivi karibuni mkoani Mwanza

"Hakuna eneo katika Wilaya za mkoa wa Mara ambalo halifai kwa uwekezaji kuanzia Tarime,Serengeti,Butiama na Wilaya nyingine za mkoa huu lakini kikubwa ambacho kitawavutia wawekezaji kuja kuwekeza ni usalama ambao utaonekana kuwepo ndani ya mkoa wa Mara.

"Kitengo cha polisi jamii mkoa wa Mara kina mipango mingi ya kukutana na wananchi katika kupeana elimu kuhusiana na masuala ya uwekezaji kikubwa wananchi watoe ushirikiano na kwa pamoja tutaufanya mkoa wa Mara kuwa salama na kupokea wawekezaji,"alisema Kanyorota.

Mkuu huyo wa polisi jamii mkoa wa Mara alisema kwa sasa wanaweka taratibu za kuhakikisha wanaunganisha madawati yote ya jinsia  yaliyopo wilayani yanafanya kazi kwa pamoja na kuweza kuwa na uwezo wa kukabiliana na shughuli zote zinazohusiana na masuala ya kijamii na jinsia

Post a Comment