0

HALIMASHAURI Kuu ya Chama cha Mapinduzi(CCM)Wilaya ya Butiama imetoa tamko la kuikataa kampuni ya ujenzi ya (CMG)inayomilikiwa na Mjumbe wa NEC Taifa Christopher Gachuma kwa kushindwa kukamilisha mradi wa ujenzi wa bwawa la umwagiliaji.

Akizungumza na Waandishi wa Habari mara baada ya Kikao cha Mkutano Mkuu,Mwenyekiti wa CCM Wilaya ya Butiama Yohana Mirumbe amesema kampuini hiyo imeshindwa kutekeleza mradi kwa wakati huku kazi ikiwa bado kubwa na hivyo kuwakwamisha wananchi.

Amesema mradi huo uliopo kwenye Kijiji cha Masinono Kata ya Bugwema kukamilka kwake kungewapa nafasi kubwa wananchi kufanya kilimo cha umwagiliaji na kuepukana na matatizo ya njaa kila mwaka lakini mkandarasi huyo ameshindwa kwenda na wakati.

Mirumbe amesema Chama cha Mapinduzi hakitashindwa kuchukua hatua na kuzifikisha sehemu husika kwa mkandarasi yoyote ambaye atashindwa kukamilisha mradi huku chama hicho kikitupiwa lawama na wananchi.

Amesema mkutano mkuu wa Chama hicho umeikataa kampuni ya Gachuma ya (CMG) kuendelea na mradi huo na kuiomba Wizara ya Kilimo na Chakula ambayo ndio iliyopitisha zabuni ya kampuni hiyo kufatilia suala hilo na kuiondoa.

Mwenyekiti huyo amesema mara kadhaa viongozi wa mkoa na chama wamekuwa wakiwasiliana na mkandarasi huyo juu ya kukamilisha mradi huo lakini ameshindwa kusikiliza na sasa hawawezi kuonea yoyote aibu bali wanataka utekelezaji wa ilani inatekelezwa.

Awali akisoma taarifa ya utekelezaji wa ilani ya uchaguzi ya CCM katika sekta ya umwagiliaji,Mkuu wa Wilaya ya Butiama Angelina Mabula amesema ujenzi wa mradi wa umwagiliaji katika kijiji cha Masinono umekuwa wa kusuasua.

Amesema mradi huo ulio chini ya DASIP uliofadhiliwa na benki ya Dunia ulitengewa bilioni 1.2 na tayari ulianza utekelezaji wake tangu mwanzoni mwa mwaka 2013 lakini mkandarasi bado amekuwa nyuma kiutekelezaji.

Katika hatua nyingine,mkutano mkuu wa CCM Wilaya ya Butiama ulitoa tamkoa pia la kuwakataa wakandarasi wawili Julias Magita na James Munubi kupewa kazi za ujenzi kwenye Wilaya hiyo baada ya kuonekana kusumbua na kushindwa kukamilisha miradi kwa wakati.

Post a Comment