0
 KATIBU TAWALA WA MKOA WA MARA BENEDICT OLE KUYAN AKIMKARIBISHA MKUU WA MKOA KUFUNGUA KIKAO CHA KUJADILI UTEKELEZAJI WA MKAKATI WA KUPUNGUZA VIFO VYA MAMA WAJAWAZITO NA WATOTO WACHANGA
 MKUU WA MKOA WA MARA JOHN TUPPA AKIFUNGUA MKUTANO HUO
 WADAU WA AFYA WAKIFATILIA

 UMAKINI UNAHITAJIKA ILI KUJADILI KUPUNGUZA VIFO VYA MAMA WAJAWAZITO WA WATOTO WACHANGA
 MKURUGENZI WA SHIRIKA LA EVIDENCE FOR ACTION  CRAING FERLA AMBAYE SHIRIKA LAKE NI MDAU MKUBWA WA KUPUNGUZA VIFO VYA AKINA MAMA WAJAWAZITO NA WATOTO WACHANGA
 WADAU WAKIWA KWENYE MKUTANO WA PAMOJA
 BAADA YA MKUTANO
 FERLA AKIJADILIANA JAMBO NA MKUU WA MKOA WA MARA
KUKOSEKANA kwa uhadilifu kwa baadhi ya wauguzi na wataalamu wa afya katika zahanati,vituo vya afya na hospitali mkoani Mara imeelezwa ndio chanzo cha kupelekea vifo vya akina mama wajawazito na watoto wachanga.
 
Kauli hiyo imetolewa na Mkuu wa mkoa wa Mara JohnTuppa alipokuwa akifungua kikao cha kupokea taarifa ya utekelezaji  mpango mkakati wa kupunguza vifo vya akina mama wajawazito na watoto wachanga mkoani Mara katika kipindi cha julai 2013 hadi januari 2014.

Amesema wananchi wengi wamekuwa wakitoa malalamiko kuhusu kukosekana kwa uhadilifu, maadili ya kazi na uaminifu na kupatikana kwa huduma mbovu ambazo zimekuwa zikipelekea matatizo kwa akina mama wajawazito na kupelekea vifo vyao na watoto wachanga.
 
Mkuu wa mkoa huyo amesema changamoto hiyo pamoja na nyingine ambazo zimekuwa chanzo cha vifo hivyo inapaswa zifanyiwe kazi na kila mmoja mwenye dhamana kwa kutimiza wajibu wake na kuwataka wakuu wa Wilaya kuwa waangalizi na wafatiliaji katika suala hilo.
 
Amesema mkoa wa Mara hauwezi kukubali kuona vifo vya akina mama wajawazito na watoto wachanga vikiendelea kutokea kutokana na uzembe wa watu wachache kushindwa kutoa huduma zifaazo za afya.
 
Tuppa amesema  Serikali  mkoani Mara imeandaa mpango unaolenga kutekeleza  mikakati iliyopo ya kupunguza vifo vya mama wajawazito na watoto wachanga ili kupata  asilimia 50 kutoka vifo 84 mwaka 2012 hadi vifo 40 kufikia mwaka 2016.
 
Amesema ili kufikia lengo kusudiwa  mkoa huo utatekeleza malengo mahususi likiwemo lengo la kusajili wanawake wajawazito na kuwafuatilia ili kuhakikisha wanahudhulia kliniki na hata wakati wa kujifungua wanakwenda kujifungulia katika vituo vya kutolea huduma vya afya sambamba na kuongeza vifaa tiba.

Akisoma taarifa ya utekelezaji wa mkakati wa nkoa kupunguza vifo vya mama wajawazito na watoto wachanga mkoa wa Mara,mganga mkuu wa mkoa Samson Wenani amesema ili kuhakikisha huduma bora zinasogezwa karibu uboreshaji vituo 13 vya afya kwa kujenga majengo ya upasuaji na kuweka vifaa tiba kwa ajili ya kuwasaidia wajawazito wanakwenda kujifungua.

Amesema majengo ya upasuaji pamoja na nyumba za madaktari wakuwasaidia wajawazito yamejengwa katika vituo vya afya vya Nyasho,Murangi,Kyagata,Iramba,Natta,Ikizu,Kasahunga,Kinesi,Muriba na Nyarwana ambapo kazi za ukamilishaji wa majengo yote katika maeneo hayo inatarajiwa kukamilika mwezi machi mwaka huu.

Kwa upande wake Mkurugenzi wa Shirika la Evidence For Action Craig Ferla ambaye kupitia shirika hilo wanaosaidia mkakati wa mkoa wa Mara kupunguza vifo hivyo alisema anashukuru mkoa kwa kudhamilia kwa dhati kuhakikisha wanapunguza na kumaliza kabisa vifo vua akina mama wajawazito na watoto wachanga ambavyo vimeonekana kutokea kwa wingi mkoani Mara.

Post a Comment