0
 
 
MAMLAKA ya Usimamizi na Udhibiti wa Mifuko ya Jamii(SSRA)umesema ni marufuku kurazimishwa kwa watumishi wa kada mbalimbali kujiunga na mfuko fulani wa jamii kwa ajili ya kujiwekea akiba na kufanya hivyo ni kinyume cha sheria ya usajili wa mifuko.

Kauli hiyo ilitolewa na Mkurugenzi wa Sheria wa SSRA Ngabo Ibrahimu katika semina ya viongozi wa halimashauri za mkoa wa Mara pamoja na wasimamizi wa mifoko ya jamii  iliyofanyika kwenye ukumbi wa uwekezaji katika jengo la mkuu wa mkoa wa Mara.

Akijibu swali la Afisa Mfawidhi wa PSPF mkoa wa Mara Sudi Hamza,Ngabo alisema kwa mujibu wa sheria ya usajili wa mifuko hiyo hairuhusiwi kwa Mkurugenzi,au mwajili katika sekta yoyote kumlazimisha mtumishi sehemu ya kwenda kujiunga na kufanya hivyo ni uvunjifuu wa taratibu.
Alisema SSRA imekuwa ikipata malalamiko kuhusiana na suala hilo na imekuwa ikitoa maagizo mara kwa mara kupinga utaratibu huo na kumuacha mtumishi kuamua mwenyewe ni mfuko gani anataka kujiunga nao.

Ngabo alisema ni wajibu kwa viongozi mahala pa kazi kuzingatia taratubu na kuona kila mfuko umeundwa kisheria na unafanya kazi sawa kwa mujibu wa sheria na kuacha tabia ya kuegemea mifuko waitakayo kwa mazoea.

Mkurugenzi huyo wa sheria wa SSRA alisema mamlaka hiyo imeundwa kwa mujibu wa sheria namba 8 ya mwaka 2008 iliyofanyiwa marekebisho na sheria namba 5 ya mwaka 2012 kusimamia sekta ya hifadhi ya jamii na ina uwezo wa kuchukua hatua kwa yoyote atakayevuruga taratibu.

Alisema licha ya SSRA kuchukua hatua kwa mifuko inayokwenda kinyume na taratibu pia wanahusika katika kutetea na kulinda maslahi ya wanachama wanaotendewa ndivyo sivyo kwenye mifuko na kuwataka wanachama kutoa taarifa SSRA pale wanapopata manyanyaso kutoka kwenye mifuko ya jamii.

Akiuliza swali katika semina hiyo iliyowashirikisha wakurugenzi wa halimashauri,miji na Manispaa,maafisa utumishi,na viongozi mbalimbali,Afisa Mfawidhi wa PSPF alidai kumekuwepo na tabia ya wakurugenzi kulazimisha watumishi kujiunga na mifuko fulani huku baadhi ya mifuko ikiendelea na tabia ya kuichafua mifuko mingine kinyume na taratibu.
Awali akifungua semina hiyo,Mkuu wa wilaya ya Musoma Jackson Msome alisema kuna umuhimu mkubwa wa kujiunga na mifuko ya jamii na kuomba elimu zaidi iendelee kutolewa kwa wananchi ili waweze kujiunga na mifuko ya jamii kwa maendeleo.








Post a Comment