0



TUME ya Uchaguzi nchini (NEC) imeomba ushirikiano kwa Vyombo vya Habari katika zoezi kuhusu maandalizi ya Uboreshaji wa Daftari   la Kudumu la Wapiga Kura litalitakaloanza hivi karibuni kwa kuhamasisha jamii umuhimu wa kujiandikisha kwenye daftari hilo.

Akizungumza kwenye mkutano  na Waandishi wa Habari mjini Musoma,Kamishina wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi Mchanga Mjaka amesema kutokana na umuhimu wa Waandishi wa Habari,Tume hiyo imeona ni vyema kuanza nao ili waweze kupata elimu na baadae watumie nafasi yao kuhamasisha Wananchi kwa kuandika Habari na Makala ili kushiriki kwenye zoezi hilo muhimu.

Amesema Wahariri na Waandishi wa Habari wana mchango mkubwa kuhamasisha wananchi na kupata taarifa ili waweze kwenda vituoni na kujiandikisha kwaajili ya Uchaguzi mkuu wa mwaka 2015 na upigaji kura ya maoni ya kupata Katiba mpya  hivyo ni vyema wananchi wakatambua umuhimu wa zoezi hilo kwa sasa.

Mjaka amesema katika uboreshaji wa daftari hilo,wapiga kura wote waliojiandisha awali na wale wapya watalazimika kwenda kituoni  kwaajili ya kuandikishwa upya kwa maana ya kuchukuliwa taarifa za kibailojia (Biometric Features).

Amesema ili zoezi hilo liweze kufanikiwa kwa malengo yaliyokusudiwa,kwa kiwango kikubwa Tume inategemea vyombo vya Habari kutokana na uwezo na hekima ya kuhamasisha jamii na wananchi kupitia vyombo mbalimbali.

Kamishina huyo wa Tume ya Uchaguzi alisema kwa kuwatumia Waandishi wa Habari wataweza kuwahamasisha wananchi kujitokeza kwa wingi katika vituo vya kujiandiskisha mara baada ya Tume ya Uchaguzi itakapovitangaza muda utakapo wadia.

Post a Comment