0


BAADHI YA VIJANA WA JIJI LA MWANZA WAKIWA KATIKA UFUNGUZI WA KAMPUNI YA BEGA KWA BEGA MICROFINANCE.
 Vijana nchini wameshauriwa kuchangamkia fursa zinazojitokeza katika maeneo yao ili waweze kumiliki  rasilimali zilizopo na kumiliki uchumi wa nchi.
Kauli hiyo  imetolewa  jijini mwanza na afisa maendeleo ya jamii damas mkama wakati akifungua huduma ya utoaji wa mikopo  kwa kampuni ya bega kwa bega microfinance 
Akizungumza kwa niaba ya fisa maendeleo wa jiji afisa vijana   juma samweli amesema hatua hiyo itawasaidia kujiimalisha kiuchumi kwa maisha yao ya sasa na baadaye.
Kwa upande wake afisa  mtendaji mkuu wa kampuni ya bega kwa bega microfinance  albert girenga amesema kuwa lengo la kampuni hiyo ni  kuwawezesha vijana wenye ujuzi na wasio na ujuzi kuweza kujiajili.
Amesema kuwa  lengo hilo litafikiwa kupitia mikopo itakayotolewa na kampuni hiyo kupitia mikopo ya anzisha  na imarisha.
VIJANA WAKIENDELE KUJIFUNZA.
Awali mkurugenzi wa ubunifu  na ugunduzi kutoka kampuni ya godtec aloyce midelo amesema kuwa  nia ya godtec ni kuinua kipato cha mwananchi  wa hali ya chini kupitia huduma ya uwezeshaji wananchi kiuchumi (poso)
Musa magari ni muuzaji wa bidhaa za mitumba amesema kuwa ukopaji wa vikundi umechangia kuwarudisha nyuma baadhi ya wafanyabishara kutoka na baadhi ya watu kutokuwa waaminifu.
UMAKINI ULICHUKUA NAFASI SANA KATIKA UZINDUZI HUO.

Post a Comment