0

Baraza  la habari  Tanzania  (MCT) limeanza kutoa mafunzo maalumu wa waandishi wa habari yatakayowajengea  uwezo wa  kuandika habari sahihi zinazohusiana na masuala ya uchaguzi mkuu unaotarajiwa kufanyika mwezi OCTOBA zitakazowapa  wananchi uwezo wa kuwapima wagombea na hatimaye kuchagua viongozi wenye sifa.

Hayo yamesemwa na ALAKOK MAYOMBO, afisa program mwandamizi  wa MCT anayesghulikia masuala ya viwango na ubora wakati akielezea madhumuni ya  mafunzo hayo yanayowashirikisha  waandishi wa mikoa ya MWANZA, GEITA, SIMIYU, KAGERA na SHINYANGA yatakayochukau siku TANO. 
 
Kwa upande wake mmoja wa wakufunzi wa mafunzo hayo, CHRIZOSTOM RWEYEMAMU katika ufunguzi wa mafunzo hayo amewahimiza waandishi wa habari kuandika habari zenye ukweli ili wajiepushe ma dhara ambayo wanaweza kukumbana nayo.,
 

Mafunzo hayo yamegawanywa katika mikoa iliyoko kwenye kanda SABA ambapo jumla ya waandishi MIA MOJA SABINI na TANO hapa nchini watanufaika na mafunzo hayo.

Post a Comment