0


MGOMBEA urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kupitia Chama cha Mapinduzi (CCM)John Pombe Magufuli,amemaliza kwa kishindo kampeni zake mkoa wa Mara kwenye uwanja wa shule ya msingi mkendo huku uwanja huo ukivunja rekodi kwa kujitokeza maelfu ya wananchi waliojitokeza kumsikiliza na kudai kutokana na imani kubwa waliomuonyesha kwa kujitokeza kwa wingi hawezi kuwaangusha iwapo ataunda serikali.
Kabla ya kuhitimisha uwanjani hapo,Magufuli amefanya mikutano ya kampeni kwenye majimbo matano ya uchaguzi yakiwemo ya Tarime vijijini,Tarime mjini,Rorya,Butiama na Musoma vijijini ambapo katika mikutano yote watu wengi walijitokeza kumsikiliza na hakushindwa kuongelea vipaumbele vyake ikiwemo suala la wanafunzi kusoma bure kuanzia elimu ya msingi hadi kidato cha nne.

Akiwa kwenye uwanja wa mkendo,Magufuli alisema amefarijika sana na umati mkubwa wa watu walijitokeza na kuahidi kutimiza maombi yaliyotolewa na mgombea ubunge wa Jimbo la Musoma mjini,Vedastus Mathayo juu ya ujenzi wa barabara za kiwango cha lami kwenye barabara za mjini na pembezoni pamoja na kupeleka kwa kasi ujenzi wa Hospitali ya Rufaa ya Mwalimu Nyerere iliyopo Kwangwa ili wananchi wapate huduma bora ya afya.

Alisema kutokana na imani waliyomuonyesha anaamini wanampa kura za kutosha pamoja na kumchagua Mathayo ili aweze kusukuma mbele maendeleo ambapo pia aliwaombea kura madiwani wanaotokana na CCM.
Baada Ya kumaliza ziara mkoani Mara,kesho Magufuli anatarajia kuendelea na kampeni mkoa wa Simiyu katika Jimbo la Busega.

 Sehemu ya umati wa wananchi
 Wakeleketwa wa CCM



 Mgombea ubunge wa Jimbo la Musoma mjini,Vedastus Mathayo akizungumza kwenye mkutano huo
 Makongoro Nyerere na Mwigulu Nchemba






Post a Comment