0


Makamu wa Rais aliwaomba viongozi wa dini zote nchini kuombea amani na kuhamasisha waumini wao kujitokeza kupiga kura oktoba 25 ili kutekeleza haki ya kikatiba na kuwasihi kukataa kushawishika na vitendo vyovyote ambavyo vinaweza kuhatarisha amani kwa kudai pasipo na amani hakuna maendeleo.


“Napenda  kuwakumbusha kwamba mwaku huu ni mwaka wa uchaguzi  na hivi sasa kampeni zinaendelea kila kona ya nchi kwa wanasiasa kujinadi kwa wapiga kura kuomba ridhaa ya wananchi kwenye uchaguzi utakaofanyika oktoba 25.

“Rai yangu kwa watanzania wote,nawakumbusha kulinda amani,umoja na mshikamano wa taifa letu kwa nguvu zetu zote na kwamba tofauti za dini,itikadi za siasa,rangi na makabira yetu yasiweze kutugawa na kila tunalolifanya tutangulize mbele masrahi ya taifa.

“Napenda kuwahakikishia,sisi ndani ya serikali tumejipanga vilivyo kuhakikisha uchaguzi mkuu unafanyika kwa amani na utulivu kwa kusimamia uchaguzi huru na haki kama ambavyo imekuwa ikizungumza kuanzia mwanzo wa mchakato huu,”alisema.




 KAIMU MUFTI WA TANZANIA,SHEK HAMID JONGO AKIENDESHA SWALA UWANJA WA SHULE YA MSINGI MUKENDO
 WAUMINI WAKISIKILIZA MAWAIDHA

Post a Comment