0
 MKUU wa mkoa wa Mara,Magesa Mulongo,kesho anatarajiwa kumuapisha mkuu mpya wa Wilaya ya Musoma,Hamphrey Polepole,baada ya kuteuliwa na Rais John Pombe Magufuli,kuwa mkuu wa wilaya ya Musoma aprili 18 kushika nafasi iliyoachwa wazi na,Zerote Stephine,aliyeteuliwa kuwa mkuu wa mkoa wa Rukwa.

Kwa mujibu wa taarifa ambazo blog ya shommi b,imezipata kutoka ofisi ya mkuu wa mkoa,zoezi la kuapishwa kwa Dc'Polepole,litafanyika kwenye viwanja vya ofisi ya mkuu wa mkoa kuanzia saa 3 kamili asubuhi na kushuhudiwa na viongozi mbalimbali na wananchi wa Wilaya ya Musoma.



Post a Comment