Waziri
wa Mambo ya Ndani ya Nchi Mh. Mwigulu Nchemba amewataka wafanyabiashara
haramu ya kuuza madawa ya kulevya kuacha mara moja biashara hiyo badala
yake watafute shughuli halali za kujiingizia kipato.
Waziri
Nchemba ametoa agizo hilo mara baada ya kuapishwa na Rais wa Jamhuri ya
Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli aliyemteua kuwa Waziri wa
Mambo ya Ndani ya Nchi Leo Ikulu Jijini Dar es Salaam kuchukua nafasi
iliyoachwa wazi na Mh.Charles Kitwanga ambaye uteuzi wake ulitenguliwa.
Aidha
Waziri Nchemba alisema kuwa atahakikisha anasimamia Ulinzi na Usalama
wa Raia na Mali zao kwa kuziba mianya inayohatarisha amani na utulivu
katika nchi.
Naye
Waziri wa Kilimo, Mifugo na Uvuvi Dkt. Charles Tizeba amesema kuwa
atahakikisha anashirikiana na wataalum wa sekta tatu zilizo katika
Wizara yake ili kufanya mapinduzi katika maeneo hayo yaliyoajiri zaidi
ya asiimia 80 ya Watanzania.
Pia
Waziri Dkt. Tizeba alisema kuwa Wizara itahakikisha inashugahulikia
changamoto zinazozokabili vyama vya ushirika ambavyo vimekuwa havifanyi
vizuri katika miaka ya hivi karibuni.
Mawaziri
walioapishwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe
Magufuli Leo Ikulu Jijini Dar es Salaam ni Waziri wa Kilimo, Mifugo na
Uvuvi Dkt. Charles Tizeba na Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi Mh.
Mwigulu Nchemba aliyekuwa Waziri wa Kilimo, Mifugo na Uvuvi anayejaza
nafasi iliyoachwa wazi baada ya Rais kutengua uteuzi wa Mh. Charles
Kitwanga.
|
Post a Comment
0 comments