MAHAKAMA ya Hakimu
Mkazi Mfawidhi Wilaya ya Musoma mkoani Mara, imewahukumu kwenda jela miaka 30
watu wawili baada ya kupatikana na kosa la unyang’anyi wa kutumia silaha (kisu)
na kupora fedha na simu moja ya mkononi aina Techno.
Waliohukumiwa kutumikia
kifungo hicho jela sambamba na kulipa fidia
ya sh laki mbili na kuchapwa viboko 24 kila mmoja ni Paulo Aloyce na Nyamuhanga Musa ambao ni
wakazi wa kata za Nyakato na Rwamlimi katika Manispaa ya Musoma mkoani Mara.
Wakati akisoma hukumu
hiyo, hakimu aliyekuwa akisikiliza kesi hiyo Richard Maganga,
alikumbushia shitaka lililokuwa likiwakabli na kusema kwamba mnamo January 24
mwaka huu majira ya saaa 3 asubuhi, mlalamikaji katika kesi hiyo Ndera Nyaki, mkazi
wa Musoma Mjini akiwa maeneo ya kiwanda cha nguo cha Musoma(MUTEX) akielekea
kanisani alivamiwa na watuumiwa na kumtishia kwa kisu kabla ya kupora vitu
hivyo.
Katika kutekeleza
dhamira yao walimpekua mlalamikaji mifukoni na kupora fedha taslimu sh 11,000
pamoja na simu moja aina ya techno vyote kwa pamoja vikiwa na thamani ya shilingi
laki moja.
Mahakama ilielezwa
kuwa, watuhumiwa katika harakati ya kukimbia mlalamikaji alipiga yowe na
kufanikiwa kuwatia mbaroni.
Watuhumiwa walifikishwa
polisi na kufunguliwa jalada la unyang’anyi wa kutumia silaha kabla ya
kufikishwa mahakamani ambapo upande wa mashitaka ulileta mashahidi watano
akiwemo mlalamikaji huku kwa upande wa watuhumiwa walijitetea wenyewe katika kesi
hiyo.
Akitoa hukumu hiyo
Hakimu Maganga, alisema Mahakama imeridhika na ushadi uliotolewa na upande wa
mashitaka hivyo watuhumiwa hao kutiwa hatiani baada ya kubainika walitenda kosa
hilo kinyume cha Sheria ya mwenendo wa makosa ya jinai Na 16 ya mwaka 2002 sura
ya 29 kifungu cha 286 na 287.
Katika
Hukumu hiyo,Hakimu wa kesi hiyo alitoa adhabu ya kifungo cha miaka 30
kila mmoja pamoja inayoendana na viboko 24 akidai makosa ya unyang'anyi
yamekithili katika Manispaa ya Musoma na adhabu hiyo itakuwa fundisho
kwa watu wengine.
Awali licha ya washitakiwa
hao kupewa nafasi ya kujitetea, bado utetezi wao haukuwa na sababu za msingi za
kuishawishi ,Mahakama hiyo iwapunguzie adhabu na ilikubaliana na hoja ya upande
wa mashitaka ulioongozwa na Wakili wa
serikali,Theophili Mazuge, wa kutoa adhabu kali ili kuwa fundisho kwa watu
wengine katika jamii.
Post a Comment
0 comments