0


SHIRIKA la Madini la Taifa(Stamico) limekusudia kuendelea na mipango mbalimbali yenye lengo la kuwasaidia wachimbaji wadogo hapa nchini ikiwa ni pamoja na kuwafanyia tafiti kwenye maeneo yao ya uchimbaji ili waweze kuchimba kwa tija.

Kauli hiyo ilitolewa na Meneja wa Uchimbaji Mgogo wa shirika hilo,Tuna Bandoma,alipotembelea mradi wa kituo cha mfano cha utafiti na mafunzo kwa wachimbaji wadogo Buhemba  kuangalia shughuli za utafiti zinavyoendelea kwenye eneo hilo.

Alisema shirika ni walezi wa wachimbaji wadogo kuhakikisha wanafanikiwa kwenye shughulizi zao na kuweza kulipa kodi stahiki hivyo kuweza kuchangia katika pato la taifa na kuimalisha uchumi kwenye familia zao.

Bandoma alisema kwa kipindi kirefu wachimbaji wdogo wamekuwa wakikabiliana na changamoto mbalimbali ikiwemo kutumia nguvu nyingi kuchimba bila ufanisi na kuja kwa mradi huu ni mafanikio makubwa kwa wachimbaji hao.

Alisema kupitia mradi huo ambao unafanyika kwenye maeneo 6 ya awali hapa nchini utatoa taarifa za kibailojia ambazo zitasaidia kutambua maeneo ambayo dhahabu na madini mengine yanapatikana hivyo kupelekea wachimbaji kuchimba kwa ufanisi.

“Uzalishaji wa wachimbaji wadogo na namna ya kusaga dhahabu tumebaini dhahabu nyingi inapotea na mradi huu unakuja kuwasaidia wachimbaji wadogo na pia yapo matumizi ya kemikali isivyo stahili yote hayo mradi huu utakuja kuyamaliza yote hayo,”alisema Bandoma.

Kwa upande wake Katibu wa Wachimbaji Wadogo mkoa wa Mara,Milele Mundeba,aliishukuru serikali kupitia Stamico kwa hatua ya kuwasaidia wachimbaji wadogo kitaalamu zaidi ili waweze kufanya kazi zao kwa ufanisi.

Alisema bila msaada kutoka serikalini wachimbaji wadogo hawawezi kufika popote na kufanikiwa kwenye shughuli za uchimbaji ili waweze kulipa kodi na kusaidia maendeleo ya familia ikiwa ni pamoja na kuwapeleka watoto shule.

Mjiolojia mwandamizi kutoka Stamico,Robert Erick,wapo katika hatua za mwisho za kukamilisha mradi huo katika eneo hilo la Buhemba na yapo matumaini makubwa ya kupatikana kwa dhahabu ya kutosha katika maeneo ambayo wameyafanyia utafiti na kuwaomba wananchi wawe na subira ya kuchimba kwa uhakika.

 Meneja Uchimbaji Mdogo kutoka Shirika la Madini la Taifa(Stamico),Tuna Bandoma(katikati),akiwasikiliza wataalam wa bailojia namna kazi ya tafiti inavyoendelea katika kuwasaidia wachimbaji wadogo kwenye eneo la Buhemba mkoani Mara.
 Wataala wakiendelea na shughuli za tafiti
 Meneja Uchimbaji Mdogo,akiangalia mawe ambayo yanatarajiwa kufanyiwa utafiti yaliyotolewa kwenye miamba

 Katibu wa wachimbaji wadogo mkoa wa Mara,Milele Mundeba,akizungumza na kuishukuru serikali katika kuwasaidia wachimbaji wadogo
 Msisitizo



Post a Comment