0




MBUNGE wa Jimbo la Bunda mjini, Ester Bulaya (Chadema) ametoa msaada wa mambo na vifungashio vyake vyenye thamani ya zaidi ya shilingi  milioni 17 ili kuweza kufanikisha upatikanaji maji kwenye Kata 7 za jimbo hilo.

Akikabidhi msaada huo kwa Mkurugenzi wa halmashauri ya mji wa Bunda kwa niaba ya mbunge huyo, diwani wa Kata ya Bunda stoo, Daud Chiruma, amesema Bulaya ameamua kutumia fedha za mfuko wa jimbo ili kuweza kukabiliana na tatizo la maji na kupunguza kero kwa wananchi.

Amesema katika mji wa Bunda na jimbo hilo kwa ujumla tatizo la maji limekuwa ni kero kubwa tangia miaka ya nyuma na tatizo hilo limeanza kushughulikiwa na mabomba hayo yataweza kusaidia kufikisha maji kwenye makazi ya wananchi.



Diwani huyo amesema msaada uliotolewa na mbunge umepokulewa na wananchi na ni vyema ofisi ya mkurugenzi ikatumia utaratibu mzuri kuhakikisha mabomba hayo yanapelekwa na kusambazwa maeneo husika ili wananchi waweze kupata maji kama ilivyokusudiwa.

 
Akipokea msaada huo, Kaimu Mkurugenzi wa halmashauri ya mji wa Bunda, Rick Kaduri, amemshakuru mbunge huyo kwa msaada uliotolewa kutokana na adha ya maji iliyopo na kuahidi kufikisha msaada huo maeneo husika na kufanyiwa kazi.

Amesema tatizo la maji ni kero kubwa iliyopo kwenye halimashauri ya mji wa bunda na kusema wataalamu wa maji katika mji huo watahakikisha wanafanya kazi ya kulaza mabomba hayo ardhini na kuwafikishia maji wananchi kama ilivyokusudiwa.

Katibu wa mbunge wa jimbo hilo, Yohana Kaunya, amesema msaada huo ni awamu ya kwanza itakayohusisha Kata 7 kati ya 14 ambazo ni Nyamakokoto,Bunda mjini,Bunda stoo,Babalimu,Manyamanyama,Nyasura pamoja na Balili na maeneo mengine yatafikiwa baadae.
 Diwani wa Kata ya Bunda mjini,Kunaga,akichimba mtaro kupitisha mabomba
 Katibu wa Mbunge,Yohana Kaunya akizungumzia msaada uliotolewa
 Diwani wa Bunda Stoo ambaye alikabidhi mabomba kwa niaba ya Mbunge Bulaya
 Wananchi wakichota maji kwenye chanzo cha maji Kata ya Bunda Stoo yanayopatikana kwa tabu ambapo msaada wa mabomba utawasaidia



Post a Comment