0


MKUU wa Wilaya ya Serengeti, Nurdin Babu, amewashutumu viongozi wilayani humo kushiriki kuhujumu miradi ya maji ili kuweza kufanya biashara ya miradi yao binafsi na kuwafanya wananchi kuendelea kuwa na matatizo ya upatikanaji wa maji.

Kauli hiyo ameitoa wakati akizindua mradi mpya wa maji wa Rain Tanzania unaofadhiliwa na Coca cola Africa Foundation na kusimamiwa na Amref ambao kukamilika kwake utawezesha Kata 4 za wilaya hiyo kunufaika kwa kupata maji safi na salama kwa wananchi zaidi ya laki moja.

Akizungumza kwa uchungu akiwa na viongozi mbalimbali wa wilaya hiyo wakiwemo madiwani,watendaji wa Kata,wakuu wa idara na wananchi,mkuu huyo wa wilaya amesema wapo viongozi ambao wamekuwa mstari wa mbele kuhujumu miradi kwa manufaa yao binafsi na kupelekea wananchi kuendelea kuumia.




 Meneja wa Coca cola mkoa wa Mara, Shabani Mshana akifatilia uzinduzi huo
 
 Mwakilishi wa Mkurugenzi Mkazi wa Amref Tanzania, James Mturi,akizungumzia mradi huo namna utakavyonufaisha jamii
Meneja mradi wa kutatua kero ya maji (Rain Tanzania) katika wilaya ya Serengeti mkoani Mara, Mhandisi Temu Japhet akizungumza kwenye hafla hiyo


 Picha ya washiriki wa uzinduzi huo wakiwa na mkuu wa wilaya ya Serengeti






 Mkuu wa Wilaya ya Serengeti,Nurdin Babu akizungumza kabla hajazindua mradi huo
 Utepe ukikatwa
 Viongozi wakifatilia uzinduzi huo



Post a Comment